THE OFFICIAL JOHN SHABANI AND GOSPEL IN AFRICA BLOG

Welcome to the official blog of the the gospel singer, songwriter and teacher John Shabani. If you are one of the fans among the millions, feel free to get connected with John Shabani and stay updated on this blog.To learn more about John Shaban and his Ministry, please click the about button above.

GET THE LATEST FROM JOHN SHABAN AND THE GOSPEL NEWS COMMUNITY

You will be able to read and review the latest news on John Shabani's tour and other specials. You will also come across the best articles of news on Gospel from all across Africa and the International Community.Please do feel free to review our categories of news and events.

FEEL FREE TO LEARN MORE ABOUT JOHN SHABANI AND HIS MINISTRY

If you wish to learn more about John Shabani and his ministry, please feel free to connect with John Shabani on the social networks. You can keep up with John Shabani and the Gospel in Africa community on both twitter, facebook, google plus and many other more.

STAY UPDATED WITH INTERNATIONAL AND LOCAL GOSPEL NEWS

Gospel in Africa Blog is a comprehensive gathering place for African Gospel music fans. Offering the latest news and information about Local and International Gospel music and news, Gospel in Africa Blog also shares the spotlight with other genres of Christian music that more than ever, seemingly overlap musical genre lines, such as Bluegrass Gospel, Christian Country and others. Singing News, the leading African Gospel and International music Blog, features African and international Gospel lyrics, radio, news, Christian concerts, songs, artists, and more.

GET IN TOUCH AND STAY CONNECTED WITH JOHN SHABANI

If you are interested in contacting and staying in touch with John Shabani then here are the contacts. E- mail: touchingvoice@yahoo.com or , princejohntz@yahoo.com, Mob: +255 754 818 767 or +255 716 560 094, www.facebook.com/john.shabani.

14 February 2017

JIAMBATANISHE NA WATU WATAKAO KUFANYA UWE BORA ZAIDI



Kuna watu wanaweza kuwa sababu ya mafanikio yako au kushindwa kwako, kuinuka kwako au kushuka kwako, kufanya vizuri au kufanya vibaya, kwenda mbali au kubaki hapo hapo!

Chunguza kwa makini watu unao ambatana nao na ikiwezekana, achana na wale wasiokufaa. Sijasema uwadharau, nimesema ujitenge nao. Wengine ni nyoka kwako wanatema sumu, wengine ni kinyonga, wanabadilika badilika, wengine ni konokono, wengine ni Mbweha, kazi yao kuharibu mizabibu, wengine ni Kuku, maisha yao ni ya chini, hivyo wewe kama Tai unahitaji kwenda juu…

Lakini pia zingatia haya;
KUWA NA HESHIMA KWA WATU WENYE MAMLAKA YA KIROHO.
Kuna maeneo 3 yenye mamlaka ya kiroho. Serikali [Taifa], Kanisa na Familia.

Heshimu maeneo haya. Kuna watu wanajikosesha baraka kwa kukosana na maeneo haya 3. Yule ambaye unadhani ni adui ktk maeneo haya matatu mpendwa wangu yamkini ndo amebeba muujiza wa kuinuliwa kwako. Daudi hakumdharau Sauli pamoja na kwamba Mungu alikuwa tayari ameshamkataa. Yusufu hakumdharau Farao au Potifa. Daniel hakuudharau uongozi wa Babeli. Maadui zako ndio waliobeba baraka zako na miujiza yako. Kwenye maeneo haya matatu usigombane nao kama wanakuchukia. Waombee na kuwatakia baraka siku zote nawe utashangaa namna utakavyokuwa ukitembea ktk kibali na neema ya Mungu.

Nakuhakikishia hebu chukua nafasi ya kuombea viongozi wako eneo lako la kazi kila siku uone mabadiliko ktk ofisi yako. Chukua nafasi ya kuombea viongozi wako wa kanisa hata kama wanakuchukia. Chukua nafasi kuwaombea wazazi wako na mwenzi wako hata kama hajaokoka na hata kama anakuchukia. Hao ndio waliobeba ushuhuda na muujiza na baraka zako mwana wa Mungu. Usiwachukie. Maandiko yanasema ‘Wala haikanushiki kabisa kwamba mdogo hubarikiwa na mkubwa’ #WAEBRANIA 7:7. Wakubwa wako hawa wamebeba muujiza wako. Waombee sasa.

Nasema asante kwa Bishop Kitonga, Mtume Fernandos, Dr. Livingstone Banjagala, Dr. Lakhan wa UK, Rose Sarwatt (Mwenyekiti wa TAWIA), Dr. Getrude Rwakatare, Askofu Jangalason, Dr. Migiro (balozi wa Tanzania Wingereza), Mh. Jakaya, Rev. Alex (Mkufunzi wangu pale ISOM na Christian Leadership University), Rev. Wilson Waidhaka (Rafiki yangu sana hapo Nairobi), Rev. Benjamin Bukuku  na wengine kibao. Hekima yenu, ushauri wenu, mafundisho yenu na maisha yenu yamefanyika msaada kwangu na kwa watu wengi.

HEART OF WORSHIP

HEART OF WORSHIP