THE OFFICIAL JOHN SHABANI AND GOSPEL IN AFRICA BLOG

Welcome to the official blog of the the gospel singer, songwriter and teacher John Shabani. If you are one of the fans among the millions, feel free to get connected with John Shabani and stay updated on this blog.To learn more about John Shaban and his Ministry, please click the about button above.

GET THE LATEST FROM JOHN SHABAN AND THE GOSPEL NEWS COMMUNITY

You will be able to read and review the latest news on John Shabani's tour and other specials. You will also come across the best articles of news on Gospel from all across Africa and the International Community.Please do feel free to review our categories of news and events.

FEEL FREE TO LEARN MORE ABOUT JOHN SHABANI AND HIS MINISTRY

If you wish to learn more about John Shabani and his ministry, please feel free to connect with John Shabani on the social networks. You can keep up with John Shabani and the Gospel in Africa community on both twitter, facebook, google plus and many other more.

STAY UPDATED WITH INTERNATIONAL AND LOCAL GOSPEL NEWS

Gospel in Africa Blog is a comprehensive gathering place for African Gospel music fans. Offering the latest news and information about Local and International Gospel music and news, Gospel in Africa Blog also shares the spotlight with other genres of Christian music that more than ever, seemingly overlap musical genre lines, such as Bluegrass Gospel, Christian Country and others. Singing News, the leading African Gospel and International music Blog, features African and international Gospel lyrics, radio, news, Christian concerts, songs, artists, and more.

GET IN TOUCH AND STAY CONNECTED WITH JOHN SHABANI

If you are interested in contacting and staying in touch with John Shabani then here are the contacts. E- mail: touchingvoice@yahoo.com or , princejohntz@yahoo.com, Mob: +255 754 818 767 or +255 716 560 094, www.facebook.com/john.shabani.

4 November 2018

KUNA VYA KULAZIMISHA VYA KUFORCE LAKINI SIO NDOA

Usilazimishe kuolewa au kuoa, usimnyenyekee mtu ili akuoe au muoane, usijidhalilishe, usijikondeshe, usitokwe na mchozi kwaajili ya kutaka mume/mke.
Utavaa nguo na kumech viatu na mkoba lakini kama MUNGU hajaruhusu uolewe na huyo huto olewa nae. Utajitaidi kumlinda, kumwezesha, kumrembesha, kama ni mkaka unajitaidi kumfanya awe mtanashati, aendane na fashion lakini kama hajaandaliwa kwaajili yako mtapotezeana muda tu.
Usijibebishe My Dear tulia Tulizana Yupo wakukunawisha Uso na Kukushika Mkono Atatoka kwa MUNGU


USITUMIE AKILI YAKO KUYALAZIMISHA MATATIZO YAKUZOEE...
Na Ukimlazimisha Mtu muoane tarajia Matusi na Dharau katika Ndoa yenu. Badala ya kujikomba, kujifanya mtu fulani wa matawi, mdada fulani hivi, badala ya kuongeza kiwango cha kurembua, kiwango cha makeup, wewe badili lifestyle yako na kuanza kuongeza kiwango cha utii kwa Mungu kisha kuomba Mungu akusaidie.

Ndoa ni kitu kizuri sana pale panapokuwapo na utayari wa mioyo ya pande zote mbili, nikimaanisha utayari wa mwanamke na mwanaume wote kuridhia kwa moyo mmoja pasipo kusukumwa kwa namna yeyote ile. Naelewa kuna nature ya Inertia (law of inertia) katika kila maisha ya mwanadamu kwamba smtms hawezi kumove kwenda hatua/sehemu ingine bila external force kuwa applied.

Ila sasa hii haiapply kwenye ishu ya ndoa. Wapo wanawake ambao mara kwa mara wamekuwa wakiforce wanaume wawaoe ili hali wao bado hawako tayari kuoa.

Wangine wanadiriki kuwashikia bango kwamba bwana usiponioa hadi mwezi fulani mimi na wewe basi, unamuimbia mwanaume wimbo wa ndoa ndoa kila kukicha kwamba utanioa lini?, hadi kufia hatua ya kuwapangia kabisa siku ya kwenda kulipa mahari.

Wengine mnatumia mbinu au makakati wa kushika mimba au kujibebesha mimba kisha kuwashinikiza kuolewa kisa mimba. Hii ni hatari sana. Unataka uolewe wewe au hiyo mimba?

Na ndio inapelekea mtu uko kwenye ndoa miezi michache tu unaanza kuichoka ndoa yako mwanaume haeleweki, kwanini? Kwa vile ulimlazimisha kukuoa wakati yeye hakuwa tayari so inamuwia vigumu kubehave like a husband.

Acha kabisa kulazimisha kupendwa, kuolewa, ukiona muda wako unaenda ni vyema ukajiondokea then ukamlingana Mungu ili akupe aliye tayari kuoa na sio kumforce akuoe. Mwanaume siku akiwa tayari kuoa utamwona anaanza yeye mwenyewe kusema sasa nataka nikuoe, siku fulani twende nikalipe mahari kwenu.

Labda huko nyuma ulikosea ukazaa na mwanaume, Kuzaa na mwanaume haimaanishi akuoe. Mwanamke hata siku moja usilazimishe ndoa. Labda kama unataka kuja kujilipua mwenyewe.

Ni ushauri wa bure kutoka kwa Brother John Shabani

25 October 2018

WATANZANIA WAKUMBUSHWA KUMUADHIMISHA MTAKATIFU YOHANA MARIA MUZEEYI (MTAKATIFU WA KWANZA TANZANIA)

HISTORIA YA YAHANA MARIA MUZEEYI
Sambamba na mahadhimisho ya miaka 150 ya uinjilishaji Kanisa Katoliki Tanzania Bara, pia tunayo kumbukumbu muhimu sana ya Mtakatifu YOHANA MARIA MUZEEYI.
Ni mmojawapo wa mashaidi 22 wa Uganda waliotangazwa rasmi na Papa Paulo VI tarehe 18 Octoba mwaka 1964 katika Mtagubo wa pili wa Vatikano kama watakatifu wa Kanisa

 Kwa ufupi ni Mtanzania aliyefia Uganda hivyo waganda wanadai alizaliwa mpakani mwa Tanzania na Uganda Kaunti ya Buddu. 
Mtakatifu Yahana Maria Muzeeyi ni mtoto wa Bahinda, amezaliwa katika kitongoji cha Kyanumbu, kijiji cha Kigazi kata ya Minziro wilaya ya Misenyi mkoa wa Kagera. Mahali hapo Minziro kuna kituo cha kitaifa cha Hija kinaitwa Kishomberwa, ni kituo cha Yohana Maria Mzeeyi na parokia ya Minziro inayoitwa jina hilohilo la Yohana Maria Mzeeyi. 
Waumini wa dini ya kikirito (RC) kutoka maeneo mbalimbali ya mkoa wa Kagera na Nje ya nchi walishiriki Missa ya Hija takatifu katika eneo la Kishomberwa,Minziro wilaya ya Missenyi.  Hija hiyo iliongozwa na Askofu mkuu wa jimbo katoriki la Bukoba Desderius Rwoma (Pichani).

Ujumbe mkuu wa siku hiyo ya hija iliyofanyika jumapili ya Januari 27,2015 ni  "tuombe Amani kwa ajili ya Taifa letu"
Askofu Rwoma akiwakumbusha waamini kuwa  Yohana Maria Muzeeyi, Shahidi ndiye Mtakatifu Mtanzania wa kwanza kutangazwa rasmi mjini Roma Italy na Baba mtakatifu Paulo VI tarehe 18th October 1964 kati ya mashahidi 21 waliotangazwa wakati huo. 27 January 2015

Ni sehemu iliozungukwa na Mto Kagera. Pia mahali hapo pamezungukwa na msitu mkubwa wenye ndege, wanyama na vivutio mbalimbali vya kitalii. Jambo lingine ni kwamba upo mlima Kabale ambapo hadi leo hii utalikuta jiwe ambalo Yohana Maria Mzeeyi alikuwa akicheza bao.
Hivyo mahali hapo ni sehemu muhimu kwa utalii wa Kidini na wa kiasili. Mamia kwa maelfu ya watu wamekuwa wakifika mahali hapo kuhiji


 Kwa uthibitisho wa haya yote basi vipo 
vitukuu vya Mt. Yohana Maria Muzeeyi vipo na wanafafanya mambo mengi muhimu tu kwa jamii, na hii ni kutokana na asili na baraka za Mungu kwa kupitia Mtakatifu huyo.


 Chakujivunia ni kwamba, huyu ndiye Mtakatifu Mtanzania aliyetangazwa rasmi kuwa mtakatifu na kanisa, hivyo ana maana kubwa sana kwa watanzania, kwa wakatoloki wote duniani na kwa kila binadamu. Hija hufanyika kila ifikapo tarehe 27 January. Hivyo basi nivizuri tukamtangaza, tukamuenzi, tukamuiga, Mungu mwenyewe alimuinua akawa mtakatifu katika maisha yetu. Wapo pia watakatifu wengine kwenye mchakato wa kutangazwa akiwemo mwalimu kambarage Nyerere na  sister Mbawala. 

HITIMISHO
Tumshukuru Mungu kwa kutujalia Mtakatifu Yohana Maria Muzeeyi, mmoja wa mashahidi ishirini na wawili wa Uganda. Ndiye Mtakatifu wa kwanza Mtanzania.
Ili kuelewa mazingira alimozaliwa, kukulia, kupata imani na hatimaye kufia ushahidi, tukumbuke kuwa zilikuwa nyakati za mataifa ya Ulaya kuvamia Afrika ili kujipatia nafasi za kufanyia biashara. Uvamizi huu ulijulikana kihistoria kama "Scamble and Partition of Africa." Katika mkutano wa nchi za Ulaya uliofanyika mjini Berlini, Ujerumani, Desemba 1884-1885, "Uvamizi wa Afrika" ulihalalishwa na kurasimishwa.
Tanganyika iliangukia kuwa chini ya himaya ya Wajerumani na Uganda chini ya himaya ya Waingereza. Lakini mipaka kati ya nchi hizi mbili haikuwa wazi na ya uhakika kama ilivyo saasa.
Mipaka ya tawala za jadi ilifuata vitenganishi asilia kama vile mito, misitu, mabonde, maziwa na milima. Hivyo, himaya ya Kabaka ilienea kusini hadi mto Kagera kama kitenganishi asilia. Ndiyo maana kata ya Minziro alimozaliwa Yohana Maria muzeeyi ilihesabika kama sehemu ya himaya ya Kabaka.
Mnamo mwaka 1890, mpaka kati ya Uganda, chini ya Waingereza, na Tanganyika chini ya Wajerumani ulisimikwa kufuata nyuzi 1 (1̊) kusini mwa Ikweta. Kwa mantiki hii mahali alipozaliwa Yohane Maria Muzeeyi paliangukia Tanganyika ambayo sasa ni Tanzania, na pamebaki hivyo hadi sasa. Hili ndilo "kosa lenye heri!" Kama si wakoloni kugawa maeneo kwa faida yao ya biashara na kutawala, Yohane Maria Muzeeyi angebaki ni Mtakatifu wa Uganda. Lakini imethibitishwa na Monsinyori Timoteo Ssemogerere aliyekuwa msimamizi wa mchakato wa kuwatangaza mashahidi wa Uganda kuwa watakatifu, kwamba Yohana Maria Muzeeyi alizaliwa Kishomberwa ya Tanzania. 
Tunapowaleteeni historia ya Mtakatifu Yohana Maria Muzeeyi, tunapenda kukariri maneno aliyosema Padre Mapeera mara baada ya kuwabatiza wakristo hao shujaa tarehe 1 Novemba 1885 katika sikukuu ya Watakatifu wote, akisema, " Tunahisi kwamba nchi ya Uganda itapata matatizo mengi. Hadi kufikia sikukuu nyingine ya watakatifu wote, baadhi ya Wakristo wapya, atakuwa wamekwisha kumwaga damu yao kwa ajili ya dini zao. Ndio mashahidi wa mbingni watakaopokelewa huko mara moja na watakuwa ni waombezi wetu. Damu yao itamwagwa juu ya ardhi hii ili iweze kuzaa wakristo wengi sana. Yesu kristo atashinda na shetanni atashindwa.Watu wengi sana wataokolewa".
Maisha ya Mtakatifu Yohana Maria Muzeeyi yanaonesha wazi kuwa ushahidi wa kumwaga damu ni kilele tu cha ushahidi wa kuvuja jasho yaani ushahidi wa maisha. Alipambana na matatizo mengi sana dhidi ya imani na maisha safi ya kikristo, hatimaye akawa mshindi hata ilipomdai kutolea maisha yake. Nao utabiri wa Padre Mapeera umetimia, Kristo ameshinda na shetani ameshindwa. Watu wengi sana wanaokolewa. Sisi tulio wazao na warithi wa imani kuu ya Mashahidi wa Uganda, hususan Mt. Yohana Maria Muzeeyi tunayo heshima na wajibu wa kuiga mfano wake. Tumfahamu uli tumuige.
Nawakaribisheni kwenye hija yetu ya kila mwaka Kituoni kishomberwa – Minziro, Jimbo Katoliki la Bukoba.
Yohana Maria Muzeeyi Ndiye Mtanzania Pekee Kutangazwa Mtakatifu
Na Askofu Methodius Kilaini (Askofu Msaidizi, Jimbo Katoliki la Bukoba)
Mtakatifu Yohana Maria Muzeeyi ni mmojawapo kati ya Mashahidi ishirini na wawili wa Uganda waliotangazwa rasmi na Papa Paulo VI tarehe 18 Oktoba 1964, katika Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatikano kama watakatifu wa kanisa. Mtakatifu Yohana Maria Muzeeyi ndiye Mtakaifu pekee Mtanzania aliyetangazwa rasmi kuwa Mtakatifu na kanisa na hivyo ana maana kubwa sana kwa Tanzania.
Katika hija ya hapo Namugongo – Kampala, nchini Uganda, mahali ambapo kiongozi wa vijana mashahidi, Kalori Lwanga, aliuawa kwa kuchomwa moto, Mhashamu Askofu Mkuu Cyprian Lwanga wa Jimbo Kuu la Kampala aliwatangazia mahujaji kwamba Yohana Maria Muzeeyi ni shahidi kutoka Tanzania na akamweleza kama kiungo cha damu kati ya Tanzania na Uganda.
Tunamshukuru sana Baba Askofu Nestor Timanywa wa Jimbo la Bukoba ambaye amefanya juhudi nyingi kukiendeleza kituo cha hija cha Kishomberwa alipozaliwa Mtakatifu Yohana Maria Muzeeyi na kufungua parokia mpya ya Minziro ili kukipa umuhimu na uangalizi. Tuna jukumu kubwa la kulinda urithi huu wa kumbukumbu ya shujaa wetu wa imani.
Nachukua fursa hii kumshukuru Padre Thomas Rutashubanyuma ambaye amekamilisha utafiti juu ya shahidi huyu shujaa kiasi kwamba sasa tunamjua zaidi na tunaweza kufuasa katika nyayo zake. Tunawashukuru vilevile kwa kutupa kimaandishi utaratibu wa ibada ya hija inayofanyika kila mwaka katika kituo hiki cha Kishomberwa. Kijitabu hiki kitasaidia sana kumjua Mtakatifu Yohana Maria Muzeeyi, kurahisisha hija katika kituo cha Kishomberwa na kueneza habari zake kwa watu wenye mapenzi mema.
Tukirudia tamko la Baba Askofu Nestor Timanywa, tunawakaribisha waamini wote kutoka sehemu zote za Tanzania, Afrika Mashariki, Afrika na dunia nzima kuja kushuhudia makuu ya Mungu hapa Kishomberwa kupitia kwa shahidi wake, Yohana Maria Muzeeyi wakati wowote lakini hasa Jumapili ya mwisho ya mwezi Januari, ikikumbukwa kwamba alifariki tarehe 27 Januari 1887.

Karibuni tuhiji, karibuni tumuige Mtakatifu huyo karibuni atuombee maisha yetu yawe ya baraka pia ili nasisi tuwezekuwa watakatifu.
Ujumbe huu umeandaliwa na:
Father Faustin Kamugisha
( Paroko wa Parokia ya Minziro)

13 October 2018

BE PART OF SHALOM ORPHANAGE CENTRE

 

I have been in Arusha and Manyara regions visiting disadvantages people and orphanage center . This my dream and vision, settled in and started volunteering at the orphanage in full force. The children are wonderful, full of love and laughter. I help the youngest kids in a way I can include raising their talents, I teach the older kids some English and then they have taken me on a few walks around the area. I had a chance to sit down and talk with the founders and local volunteer to learn more about the organizations. Here is the inspirational yet heart wrenching story.

One of the interest center is shalom orphanage center:
Mama Warra is an amazing lady and the children and staff at Shalom are full of love.
Mama Warra wants to empower these children to know how important it is to continue to help and sharing to others what they have. These children have no desk top or laptop computers, no video games new clothes and on Christmas Day they go into town to meet the street children and bring them food, pencils, clothes, and toys – all items that were donated to them and they then share these gifts and give them to other children who do not have a place like Shalom, they call it “Celebrate Christmas Donated By Shalom.” 

Shalom believes that every child has a dream and it is their hope to give these children an opportunity to use their skills and gifts to reach their full potential and see their dreams become reality. They can’t do this on their own there is a high demand for support.

How you can help
Financial and Material Support: 
• There is a high demand to purchase items on their daily wish list including food, first aid supplies, tooth paste and brushes, cooking oil, soap, medical care, etc.
• Contribute to the construction costs of upkeep to the current building, a hope for a new school, community houses and volunteers house.
• Help with the cost of utilities
• Contribute academic materials such as backpacks, school supplies, and books
• Volunteer! 

Shortly about SOC
The Shalom Orphanage Centre is located in a small town called Karatu in Tanzania which is about a two hour drive from the airport, and very close to the Ngorongoro Crater safari destination. It’s in a lush green valley, down a dirt road away from the main town.The orphanage is currently home to 75 children, aged between 1 and 14 years old. It was founded by Mama Nnko in 2004 and has grown a lot since then. 

The orphanage sits on a two acre plot of land that was donated by an NGO and comprises a number of buildings where the children eat, sleep, are schooled and play. 

Every child has a dream and it is our hope to give our children opportunity to use their skills and gifts to reach their full potential and to see their dreams become reality. We ensure each child receives love, food, shelter, education and medical care. We believe, through education we can combat disease, eliminate poverty and enable our children to grow up in a HIV/AIDS and starvation free society.

Most of the children arrive at Shalom due to either lack of parental care through the death of their parents or abandoned. This is due to low-level economic strategies, rapid growth of HIV/AIDS, alcoholism and the decline of the family structure. Also, the majority live under national poverty line due to lack of employment opportunities and access to education whereby in one way or another may lead to increase in the number of street children and orphans.

You are invited to work with hand in hand with us. 
Join me to bring hope to these beautiful and handsome kids.

For more information: +255716560094, +255754818767, +255755244117 
Email: jshabani2011@gmail.com or shalomchildren2006@yahoo.com  


31 July 2018

JINSI YA KUZUNGUMZA NA KUMTULIZA MPENZI ALIYEKASIRIKA


Uatake usitake kwenya Mapenzi kuna makati za kutofautiana, kukasirishana... Kipindi hiki huwa ni cha hatari sana maana kinaweza kutengeneza nyufa kwenye mahusiano yenu.

Sote tunajua, watu hupigana, huachana, hujeruhiana, hutukanana, hudhalilishana wakiwa na hasira. Hata hivyo si wote wanaojua wafanye nini wanapojikuta wameingia kwenye hatua hiyo mbaya.
Msomaji wangu, hebu jaribu kukumbuka ugomvi mmoja uliotokea kati yako na mpenzi wako na ikiwezekana jikumbushe mlivyoanza! Utabaini kuwa mlianza kama utani na mkajikuta mmefura kwa hasira, mkatwangana makonde, mkatamkiana maneno makali ya kuudhi na pengine mkaamua kuachana.
Yote hii ni kwa sababu mlikosa ELIMU YA MAZUNGUMZO. Ingekuwa mmoja wenu hasa yule aliyekuwa wa pili kukasirika anafahamu hatua za kuzungumza na mtu aliyekasirika angechukua jukumu la kutuliza machafuko na kuleta amani kwenye mapenzi. Tazama hatua tano za kuzungumza na mpenzi aliyekasirika.

MPUNGUZE MHEMKO
Hasira hujaza kifua, huathiri mzunguko wa damu na ufahamu. Mtu aliyekasirika huwa vigumu kwake kusikiliza au kutazama mambo kwa jicho la tatu. Mwenye hasira huwa hafikirii matokea yajayo badala yake hutazama zaidi tukio na jinsi ya kupata ushindi iwe kwa maneno au kwa mapambano.
Katika hali ya namna hiyo, mtu mwingine akija na busara za kutaka kumgeuza haraka haraka hawezi kumuelewa. Muhimu hapo ni kuacha kumwadama, kujibizana naye, kumshawishi asikilize badala yake mpe nafasi ya kusema atakavyo, abwate ajuavyo huku wewe ukimuitikia na kumkubalia lawama zake. “Basi mpenzi mwenye makosa ni mimi.” Kauli za aina hii zitampunguza hasira kwani atajiona msindi.

MSOME SAIKOLOJIA YAKE
Kwa kuwa unamfahamu mpenzi wako kwa kina itakuwa rahisi kwako kumtambua kuwa amepunguza hasira na kurudi katika hali yake ya kawaida. Ukisha fahamu hilo chukua jukumu la kumsoma kisaikojia ili kujua kama yuko kwenye hali nzuri ya kusikiliza yale uliyotaka kumwambia wakati alipokuwa na hasira.
Zoezi hili linaweza kuchukua saa kadhaa na wakati mwingine hata siku mbili. Lengo ni nini? Ni kupata matokeo sahihi ya kuondoa chuki za mwenza wako na kumfundisha madhara ya kukasirika kwenye uhusiano wenu wa kimapenzi. “J, nakupenda sana, lakini juzi uliniumiza, uliniambia mimi malaya kwa kosa ambalo sikufanya?” Bila shaka muda huo atakusikiliza zaidi kuliko ungebishana naye alipokuwa na hasira.

MRUHUSU AKUJIBU
Pamoja na kumsoma kisaikojia na kumwambia kinagaubaga makosa yake, usimzuie kujitetea, mpe nafasi ya kuzungumzia kilichomkasirisha. “Unaona bado unanitukana, sasa naamini siku ile ulikuwa umedhamilia.” Usisiseme hivyo, mwache ajibu hoja hata kama atakuwa anakukandamiza na kuzidi kujijengea ushindi. Mvumilie aoshe ubongo wake.

EPUKA MARUMBANO
Kama nilivyosema kwenye hapo juu, wapenzi wengine huwa wagumu kuelewa, ni watu wa kuficha udhaifu wao na kutopenda kuonekana wamekosea. Watu wa namna hii unapowarejeshea mazungumzo wanaweza kujikuta wanahamaki tena.
“Kwa hiyo ulikuwa unasemaje…nilifanya ndiyo,… wewe unaamuaje?” Mkifika kwenye alama hiyo usikubali kurumabana naye mwache aseme halafu wewe ingia kwenye hatua ya tano.

MUOMBE MSAMAHA
Hata kama atakuwa yeye ndiye mwenye makosa na amekataa kukiri, usijali, chukua jukumu la kumuomba msamaha na kueleza tena nia yako ya kumazungumzo ilikuwa ni kuelewana si kugombana. Kumbuka hata kama amekiri kosa, bado unatakiwa kumuomba radhi kwa kurejea yaliyopita. “Mpenzi inawezekana nikawa nimekuudhi kwa niliyosema, nakuomba sana tusameheane.”
Bila shaka kwa haya machache msomaji wangu utakuwa umejifunza na kuchukua hatua za kuzuia migogoro mikubwa inayotokana na hasira za mpenzi wako.



28 June 2018

SIKU YA TUKIO KUBWA LA WATANZANIA WOTE KUKUSANYIKA PAMOJA KUMSIFU MUNGU




 WAPENDWA, ILE SIKU YA WATANZANIA WOTE BILA KUJALI DINI ZAO AU DHEHEBU, KUKUSANYIKA PAMOJA KUMSIFU MUNGU WETU IMEFIKA SASA.
NAWAKARIBISHA RASMI ILI TUMTUKUZE MUNGU WETU.

 NI SIKU YA UJIO MPYA WA PST. JOHN SHABANI, YULE MWALIMU MAARUFU 
WA NYIMBO ZA INJILI ALIYEFUNDISHA KWAYA NYINGI NA WAIMBAJI WENGI BINAFSI. 
JOHN SHABANI ATAWAONGOZA MAMIA YA WATU KATIKA KUSIFU, 
PIA SIKU HIYO DVD YAKE ILIOANDALIWA KWA VIWANGO ITAWEKWA WAKFU. ZAIDI YA KWAYA KUMI NA WAIMBAJI BINAFSI WATAHUDUMU. 








NI PALE NDANI YA KANISA LA WCC KEBBY'S HOTEL MWENGE MKABALA NA KITUO CHA ITV. NI TAREHE 1/7/2018, KUANZIA SAA NANE MCHANA.
NI TUKIO LITAKALOHUDHURIWA NA MAASKOFU, WACHUNGAJI, MITUME NA WATU WA DINI ZOTE.MGENI RASMI NI MISS NGUSE NYERERE, WAGINI MAALUM NI MADAME LUUNDO KUTOKA CANADA NA MCHUNGAJI NA MWALIMU PETER MITIMINGI, ATATOA UJUMBE MAALUM KWA WAIMBAJI NA KWA KILA MWENYE KIU YA KUMTUMIKIA MUNGU. 
HAKUNA KIINGILIO, NJOO NA ELFU KUMI KWAAJILI YA KUNUNUA DVD. RANGI YA TUKIO NI NYEUSI NA NYEKUNDU
KWA MAWASILIANO ZAIDI 0759778778 NAMAANISHA 0759778778 
NJOO WEWE NA RAFIKI ZAKO, PIA NISAIDIE KUSHARE TANGAZO HILI.

15 June 2018

TUKIO KUBWA LA UZINDUZI WA WCC CHOIR, KWAYA YA KANISA LA WAREHOUSE CHRISTIAN CENTRE (GHALA LA CHAKULA) LINALOONGOZWA NA MCH. NA MWL. PETER MITIMINGI

Zawadi pekee ya kwaya kwa baba na mama
Mwalimu John Shabani, Mtumishi Peter Mitimingi, saa ya kuabudu.




 Hawa ni mamia ya watu waliohudhuria siku ya tukio.
 Praise team ya kanisa wakimtukuza Mungu

 Baada ya tukio lililotikisa jiji la Dar es salaam na Tanzania kwa ujumla la uzinduzi wa kanisa "GHALA LA CHAKULA - WARE HOUSE CHRISTIAN CENTRE", baada ya miezi michache limefanyika tukio lingine kubwa zaidi ndani ya kanisa hilo, si ligine bali lile la uzinduzi wa kwaya pekee ya kanisa hilo (WCC CHOIR).

Hakika haijawahi kutokea kwa kanisa linaloanza kuwa na kwaya ya zaidi ya watu 50, tena wakiimba kwa ufanisi wa hali ya juu. Hii ni kutokana na mafunzo maalum kutoka kwa mtaalam wa sauti na mwalimu John shabani. Ni kwaya pekee yenye watu wa rika zote.

Tunasababu zote za kumpongeza Mtumishi Peter Mitimingi kwa maono haya makubwa ya kuanzisha huduma itakayoleta ukombozi kwa jamii.

HACK MOYO WA MPENZI WAKO USIHACK SIMU YAKE - UJUMBE MUHIMU KWA WANANDOA NA WALIO KWENYE MAHUSIANO

    Huu ni ujumbe muhimu kwa wanandoa na walio 
kwenye muhusiano kutoka kwa
Winnie Nzobakenga

Nimewahi kusikia wanawake wengi wanaulizia jinsi ya kuhack simu za waume zao ili wawe wanasoma meseji za waume zao. Haya yapo pia hata kwa wachumba.  Mmh! hivi ninyi wamama au wan awake wenzangu, mnajipenda kweli? Sasa ukishahack simu yake then what?

Ukikuta msg za wanawake wengine then what,inakusaidia nini??ukishajua mmeo anamchepuko utachukua mapanga na visu na panga kwenda kupigana?utaweza kweli?ukishajua kuna mwanamke kazaa naye na amempangishia nyumba utapata nguvu za kwenda kumpiga huyo mwanamke?? Ukishajua utaongeza mapenzi kwa mme wako au ndio utaenda kuvunja ndoa na kubeba vilago na kuondoka?watoto utaawaacha au utaondoka nao,nani atawalea,nani atawapa matumizi??ninawambia kabisa ninyi ambao mnahangaika kujua namna ya kuhack simu ya mme wako kujua kinachoendelea.
NISIKIE NIKWAMBIE
Hapo tatizo sio simu,tatizo ni moyo ,unatakiwa udeal kuurudisha moyo wake.Ukihangaika na simu,simu haina shida wanaweza wakaacha kuwasiliana mme akahamia kabisa kwa mchepuko utamfanyaje?mbona simu ni kitu kidogo saaana.Wewe fanya juu chini huo moyo wake usikuponyoke,moyo ukishaponyoka hata uhack nini hamna kitu. Kuna mwingine anataka akishakuta msgs kwenye simu ya mme wake ndio aanze kufunga na kuomba,kuombea ndoa yake.Sikia tu nikupe siri sio rahisi kuomba ukishajua kuna anayekuzunguka utachemsha,utaishia tu kulia.Askari yeyote huwa hafanyi mazoezi siku ya vita,siku ya vita huwa anaenda kufanya alichofanyia mazoezi miaka au miezi kadhaa iliyopita ya maandalizi.
Huna haja ya kukamata msgs za mapenzi za mwenzi wako ndio uanze kuomba,anza kuomba sasa,wewe omba kabisa kwa nguvu zako zoote.Biblia inasema kuwa "Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa.(1 Wathesalonike 5:3). Kumbe kati ya watu wanaotakiwa kuombea ndoa zao kwa mzigo mkubwa ni wale ambao saivi wanaona kuwa ndoa zao zina amani.Amani uliyonayo na furaha visikufanye ukajisahau na kulala omba omba hayo maombi yatatumika wakati wa vita.Wala haina haja ya kukuta msgs za mcheps ndo uanze kuomba .Yafanye maombi kuwa maisha yako,usiishi bila maombi,usiongeje maombi ya zima moto. Jambo jingine Biblia inasema kwamba Aogopacho mtu asiye haki ndicho kitakachomjilia; Na wenye haki watapewa matakwa yao.(Mithali 10:24)
Kuna wanawake wao masaa 24 wanawaza kuhusu michepuko,hawana imani kabisa na waume zao,kila wakati kila saa anawaza mme yuko na mtu mwingine,akichelewa tu kurudi nyumbani anawaza mme wangu yuko kwa mwanamke,simu ya mwanaume isipopatikana tu kidogo hewani mke anajua mme yuko kwa mchepuko,pesa asipoona matumizi yake anajua kapewa mchepuko. Yaani mwanamke anaishi hayo maisha ya wasiwasi wakati wote utafikiri kuku mtetea anayetafuta sehemu ya kutaga.Mara ashike simu ya mme atafute msgs na dialled calls na received calls,mara aende kwenye messenger ya facebook na whatsup,mara atafute jinsi ya kuhack number ya mmewe,mara anunue number mpya aanze kumtumia mmewe msgs na kujifanya mwanamke mwingine ili mradi tu afanye fujo.Mme akirudi ananuswa hadi nguo za ndani hadi mdomo utanuswa hahaha utafikiri mbwa wa usalama,kwa madai ya kuwa mke ni mlinzi.
Rafiki wala hatulindagi hivyo,ulinzi ni kufanya majukumu yako kama mke na kusugua goti.Hayo mengine mwachie Mungu ashugulike naye,ukisugua vizuri goti hakuna kitu ambacho kitafanyika kinyume Mungu asikujulishe.Lolote kabla halijatokea ktk ulimwengu wa mwili,Mungu atakuonyesha ktk ulimwengu wa roho na utakisambaratisha kabla hakijatokea juu kwa juu.Ndio maana nasema usighulike sana kwa namna ya mwili kuhack sijui simu na msg,shugulika magotini.Kuna mambo ukiyafanya kwa mmeo automatically utauhack moyo wa mwanaume na kikubwa ni #Unyenyekevu.,vingine nitakupa siku nyingine.Ila ukweli ni kwamba unaweza kuuteka moyo wa mmeo,kama Delila aliweza na wewe unaweza.Stop hacking your husbands phones,kwanza huo muda mnapata wapi??
Winnie Nzobakenga

6 June 2018

MWALIMU NA MCHUNGAJI DKT. PETER MITIMNGI AANZISHA HUDUMA IJULIKANYO KWA JINA LA GHALA LA CHAKULA - WCC

 Baada ya kulitumikia kanisa la TAG kwa miaka mingi kama mchungaji msaidizi na baadaye kuanzisha huduma ya injili vijijini - VHM, hatimaye Mwalimu na Mchungaji Peter Mitimingi aanzisha kanisa lijulikano kwa jina la Ghala la chakula au kwa kimombo; Warehouse Christian Centre - WCC
 Mchungaji Peter Mitimingi akiwa katika picha ya pamoja na wahudumu siku ya uzinduzi wa kanisa.
 Maelfu ya watu waliohudhuria siku hiyo


Na John Shabani - Dar es salaam

Baada ya kutumika katika kanisa la Tanzania Asseblies of God  (TAG ) zaidi ya miaka ishirini Mchungaji na mwalimu Dr Peter Mitimingi azindua kanisa lake rasmi  Kebbys Hotel Jijini Dar es salaam.

Akizungumza katika uzinduzi wa kanisa hilo uliohudhuriwa na zaidi ya watu elfu tatu  Dr Mitimingi amesema kuwa yapo malengo matatu ambayo yamepelekea yeye kuanzisha WCC ikiwa ni pamoja watu kukua kiroho ,wawe na Ufahamu,waijue kweli ambao utamsafirisha kupata majibu ya changamoto mbalimbali pamoja na Uhuru

Amesema kuwa wengi waneokoka na wapo makanisani miaka mingi lakini hawajakua kiroho,amesema kuwa mtu akilifahamu tatizo ni jibu sahihi kuliko kutokujua tatizo.

"Kwakutolifahamu tatizo unaweza ukatibu ugonjwa ambao siyo kabisa ila ukilifahamu tatizo utajua uanzie wapi kulitatua,kwani ratizonlinaanzia kwenye kulijua tatizo lenyewe " alisema Mitimingi

Ameeleza kuwa katika malengo hayo endapo angeendelea kuwa katika kanisa la TAG malengo hayo yasingekamilika kutokana na taratibu za Kanisa hilo.

"Sijatoka kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG )kwa ugomvi kama watu wanavyozusha bali nilikwenda kwa viongozi wa juu wa Kanisa wakanisa nilianza na nyumbani Mwenge TAG
ambapo nilikuwa mchungaji msaidizi, nikaenda kwa mchungaji wa wilaya , nikaenda kwa Makamu wa Askofu Mkuu wa kanisa la TAG Dkt. Magnus Mhiche ,wote hawa walinikubali ,wakaniombea na kuniwekea mikono tayari kwa kutumika." Alisema Mitimingi.
 

Mungu akubariki Mtumishi kwa maono haya makubwa.

HEART OF WORSHIP

HEART OF WORSHIP