Pages

28 May 2021

FAIDA ZA KUIMBA



FAIDA ZA KUIMBA

Kuna aina mbili kuu za faida:

1.              Faida za kuimba ambazo zinamsaidia mtu kiafya.

2.              Faida za kuimba kwenye jamii

Kwanza kabisa naomba nikueleze maana ya kuimba. 

KUIMBA ni kutoa sauti yenye ulinganifu, sauti hiyo inatakiwa kufuata mapigo ya ki muziki na ni zaidi ya kughani. Zamani mababu zetu walikuwa wanaimba kwenye kazi mbalimbali ili kurahisisha kazi yenyewe iliyokuwa ikifanyika, mpaka sasa watu wengi huimba ili kuburudisha, kufundisha, kukosoa au kuelimisha kikundi fulani cha watu.

Kuimba ni faida kwa mwimbaji kwani kuna faida nyingi saana ambazo mwimbaji anazipata kama vile kuburudika, kuburudisha, kuinjilisha, kuhamasisha, kufariji, kufurahisha n.k

Leo nitakueleza faida za kuimba ambazo zinamsaidia mwimbaji kiafya:

  1. Kuimba ni mazoezi. Unapoimba unafanya mazoezi ambayo pia ni kinga kwa magonjwa mbalimbali yanayoweza kumuathiri mtu ambaye hafanyi mazoezi. Mazoezi ambayo nayasemea hapa ni Kupanua kiwambo (diaphragm), mwanakwaya anatumia nguvu nyingi sana wakati anaimba ili kupanua mapafu na kiwambo. Hii itamsaidia mwimbaji ku zuia magonjwa yanayoweza kuathiri mapafu kama vile kikohozi, mafua.
  2. Inasaidia kuboresha mfumo wa upumuaji mwilini kwani msukumo wa damu utakuwa mkubwa ambapo ndani ya chembe za damu huwa kuna hewa safi ya Oxygen ambayo husambazwa mwilini pote na chembe za damu katika mzunguko. 
  3. Inasaidia kupunguza mawazo. Hili liko wazi kabisa  kwa mwanakwaya au mwimbaji yeyote yule, ukiimba unapunguza mawazo. Mtu mwenye mawazo anaweza kuugua hata magonjwa ya akili na kisaikolojia.
  4. Husaidia kusimama vizuri. Mwimbaji huwa ana staili yake ya jusimama ambapo kifua chake anakiweka mbele, mabega yanakuwa yameinuka kidogo ili kumsaidia kutoa sauti, mgongo pia unakuwa umenyooka vizuri. Hii inamsaidia kuufanya uti wa mgongo usijikunje. Kwa hiyo mwanakwaya anapoimba kwa muda mrefu huwa na tabia ya kusimama kama anataka kuimba na hivyo kumsaidia yeye kutunza na kukinga uti wa mgongo.
  5. Huimarisha mfumo wa kinga mwilini. (strengthen the immunity system) Kwenye mwili wa binadamu kuna kinga (protini) ambayo ina jina la kitaalamu ambalo ni Immunoglobulins, kwa hiyo mtu anapoimba anafanya mazoezi (kama nilivyosema hapo juu) na unapofanya mazoezi ina maana kwamba unaongeza kinga mwilini tofauti na mtu ambaye amekaa tu bila kufanya mazoezi


Kwa ufupi sasa kuimba kuna faida kiafya, faida zingine nimezitaja hapa chini ambazo ni:

  • Kuimba nidawa ya asili ya mawazo (natural annti-depresant)
  • Kuimba kunapunguza mawazo kwa kiasi kikubwa sana (ni dawa kwa mtu mwenye mawazo)
  • Kuimba kunaongeza uwezo wa kufikiri na kuchukua maamuzi.

Faida za kuimba kwenye jamii.

Kuimba humsaidia mtu kuongeza idadi ya marafiki.

Kuimba kunamwongezea mtu kujiamini katika kila kitu anachokifanya kwa faida yake na jamii kwa ujumla.Kuimba kunapanua wigo wa mawasiliano.

Lakini zaidi ya hapo kuimba ni ajira kubwa.

Naamini masomo haya yamefungua ufahamu kwako. Ukitaka kujifunza zaidi tuwasiliane, ili nawewe uwe mmoja wa wanafunzi wangu katika darasa letu la mafunzo ya sauti na uimbaji.

Whtspp/call +255716560095

Facebook: John Shabani (Mtoto wa Mfalme)

Instagram: sjvocaltraining

E-mail: jshabani2011@gmail.com

Web: www.johnshabani.blogspot.com

No comments:

Post a Comment