3 February 2015
HATIMAYE CHINI YA USIMAMIZI WA MWL. JOHN SHABANI WATOTO WA SHALOM ORPHANAGE WAREKODI ALBAM YAO YA KWANZA
22:07
No comments
Mwl. John Shabani akitoa darasa
kwa watoto wa Shalom Orphanage
Nilitembelea
kituo cha Shalom Orphanage Centre mwaka 2014, hakika nilijifunza mambo mengi,
huku nikijaribu kuona tofauti iliopo kati ya vituo mbalimbali vya watoto yatima
nilivyowahi kuvitembelea Tanzania na nje ya mipaka yetu.
Mlezi wa
kituo hicho Mama Warra Nnko, kwanza ni Mjane, pili baada ya kuguswa na haili ya
maisha ya watoto yatima, aliamua kusahau hali yake ya ujane na kujiona kuwa
anayo nafasi kubwa ya kufanya lolote awezalo ili kuyakomboa maisha ya mtoto
yatima Tanzania. Ndipo Mama huyo alipoamua kutoka katika Jiji la Arusha, huku
akiacha makazi yake mazuri na kujielekeza huko karatu, ni takriba kilomita 160
kutoka Jiji la Arusha. Tangu mwaka 2004 Mama huyo akilea watoto yatima
katikamakazi aliyofanikiwa kuyapata huko karatu. Ukifika Shalom Orphanage Centre
hakika huwezi kuyazuia machozi yako, hasa bale unapoona zaidi ya watoto 60, wengine
wachanga, wengine wenye ulemavu, wengine walioathirika na ukimwi, wote hao
humwita Mama warra jina moja tu (Mama)
Ikumbukwe,
jirani na wilaya ya karatu ndiko kunakoongoza kwa vivutio vya utalii
Tanzanzania, hivyo, kwasababu ya habari zilizoeneo kote duniani kuhusu kituo
hicho, watalii na wasamaria wengi wanaotembelea Ngorongoro, Serengeti, n.k,
mara nyingi pia hukitembelea kituo hicho.
Niliposikia
habari za kituo hicho, nikiwa mwana harakati wa haki za Binadamu, nilifunga
safari na kutembelea shalom Orphanage, nikajisikia kunzisha program ya kuibua
vipaji hasa vya uimbaji. Kwa kuanzia, tayari mapema mwaka huu wa 2015, tumerekodi
Albam ya kwanza na maandalizi ya mkanda wa video yanaendelea. Naamini kwa
kupitia ujumbe uliomo ndani ya nyimbo hizi utagusa mioyo ya watu wengi ndani na
nje ya nchi. Lakini pia mkanda wa video utakiunganisha kituo na dunia, kwani
nyimbo hizo zitatafsiriwa kwa lugha ya kingereza. Pia nyimbo hizi zitawaingizia
kipato.
Baadhi ya
nyimbo zilizomo katika Albam hiyo ni: Mtoto
wa mwenzio ni wako, Sitaitwa Yatima tena, Nani kama Mama, Baba wa Yatima na
Tanzania.
Endelea kuombea kituo hicho, na pia unaweza ukatoa
mchango wako wa hali na mali ili kuwabariki watoto hao.
2 January 2015
JOHN SHABANI NA ZIARA YA KUTEMBELEA VIVUTIO VYA UTALII WA TANZANIA PAMOJA NA KUIBUA VIPAJI VYA WATOTO
21:37
No comments
Nikiwa na watalii mbalimbali karibu na mto wa ajabu, baada ya kuzunguka kutwa nzima eneo la Ngorongoro Crater, watalii huja mahali hapa penye idadikubwa ya viboko.
Imekuwa ni ziara ya kipekee kati ya ziara nilizowahi kuzifanya. Kwani nimejionea moja ya maajabu ya dunia, Ngorongoro Crater. Pia nimeweza kuibua vipaji vya watoto pamoja na kurekodi nyimbo kadhaa.Ngorongoro ("Ngorongoro Conservation Area") ni umbali wa takribani kilomita 180 kutoka Arusha na pia hifadhi ya taifa inayojulikana kote duniani. Eneo hili ni sehemu ya Serengeti.
Kuna
jumla la wanyamapori
wakubwa takriban 25,000, wakiwa pamoja na vifaru, viboko, nyumbu, pundamilia, nyati, simba,
fisi
na chui .
Ngorongoro
imepokelewa katika orodha ya urithi wa dunia ya UNESCO.
|
Je unajua kitu kuhusu Ngorongoro kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? |
Pia, kuna
Ziwa Magadi ndani ya bonde refu na kubwa maarufu kwa jina la ‘Ngorongoro Crater’
lililosababishwa na milipuko ya volcano zaidi ya miaka 2000 iliyopita.
Mahali
hapo si pengine popote, ni Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (Ngorongoro
Conservation Area Authority – NCAA) iliyoanzishwa mwaka 1959 na kukabidhiwa
majukumu makuu yafuatayo:
Kuhifadhi
maliasili (wanyamapori, ndege na mazingira) zilizopo, kuendeleza binadamu
wenyeji (Wamaasai) na utalii katika hifadhi hiyo.
Ina eneo
lenye ukubwa wa kilomita za mraba 8,292, inapakana na Hifadhi ya Taifa ya
Serengeti (SENAPA) upande wa Kaskazini Magharibi na miji ya Arusha, Moshi na
Mlima Kilimanjaro upande wa Mashariki. Maelfu ya watalii kila mwaka kutoka pembe nne za dunia hutembelea Ngorongoro.
Nikiwa na watoto wa Shalom Orphanage center baada ya kukaribishwa kula chakula katika hotel ya Sarena
John Shabani, watoto wa Shalom na rafiki zetu wengine
Nikiwa na kundi kubwa la watoto baada yakupata chakula katika hotel ya Serena
1 December 2014
NI MSIBA TENA KWA JOYOUS CELEBRATION
21:07
No comments
Mwimbaji Marehemu Lihle Mbanjwa akiimba kwa hisia katika ya matukio ya uimbaji ya kundi hilo mwaka jana
Our drummer Sabu Satsha was travelling in the same car suffered head injuries and is critical but stable in Hospital. A relative of Lihle who was also in the car is also admitted at a hospital and he is in a stable condition.
We appreciate your continued support over the years.We are counting on your prayers and support during this difficult time for us and their families.
God bless you.
26 November 2014
WAJANE WAANZA KUNUFAIKA NA CHAMA CHAO
20:53
No comments
Wajane wakiwa wametulia nje ya ofisi za chama, huku wakimsikila mwenyekiti
Mwenyekiti akisaidia kubeba viti
Wajane wakigonganisha vinywaji vyao na mwenyekiti kwa kutakiana afya njema
Ni mkutano mwingine wa wajane, wakijadili mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja
na kuimarisha umoja huo.
Akionekana mwenye uso wa furaha, mwenyekiti wa chama hicho ambaye kabla ya
kikao kuanza alijitolea kubeba viti na kuvipanga, amewapongeza wajane kwa
kuendelea kujitokeza kwa wingi kujiunga na chama. Pia kwa juhudi zake
mbalimbali, zipo shule pamoja na
wafadhili mbalimbali wamekubali kuwasomesha watoto wa wajane. Wito wa
Mwenyekiti ni kuziomba shule mbalimbli kukukubali kuwasomesha watoto wa wajane.
Katika mkutano huo uliofanyika nje ya ofisi za Chama cha Wajane Tanzania ,
maeneo ya kinyerezi Dar es salaam, wajane pia wamenufaika na misaada kutoka kwa
wadhili mbalimbali ikiwa ni pamoja na mavazi, chakula, sukari, mchele pamoja na
sabuni.
Mkakati mkubwa sasa ni kuhakikisha kila mjane anasaidiwa kupata mtaji ili
kuwa na shughuli binafsi ya kumwingizia kipato, ili kujikimu kimaisha. Maana
lengo kuu la chama ni
kurejesha matumaini ya wajane.
Wito ni kwa wajane wote Tanzania kujitokeza kujiunga na chama hicho
kilichosajiliwa kihalali. Pia mlango uko wazi kwa wafadhili wa ndani na nje,
taasisi mbalimbali, matajiri na wakereketwa kujitokeza kusimama na wajane na
kuwasaidia kwa hali na mali.
Mkakati sasa ni kukieneza chama nchi nzima.
Subscribe to:
Posts (Atom)
HEART OF WORSHIP














.png)

















