THE OFFICIAL JOHN SHABANI AND GOSPEL IN AFRICA BLOG

Welcome to the official blog of the the gospel singer, songwriter and teacher John Shabani. If you are one of the fans among the millions, feel free to get connected with John Shabani and stay updated on this blog.To learn more about John Shaban and his Ministry, please click the about button above.

GET THE LATEST FROM JOHN SHABAN AND THE GOSPEL NEWS COMMUNITY

You will be able to read and review the latest news on John Shabani's tour and other specials. You will also come across the best articles of news on Gospel from all across Africa and the International Community.Please do feel free to review our categories of news and events.

FEEL FREE TO LEARN MORE ABOUT JOHN SHABANI AND HIS MINISTRY

If you wish to learn more about John Shabani and his ministry, please feel free to connect with John Shabani on the social networks. You can keep up with John Shabani and the Gospel in Africa community on both twitter, facebook, google plus and many other more.

STAY UPDATED WITH INTERNATIONAL AND LOCAL GOSPEL NEWS

Gospel in Africa Blog is a comprehensive gathering place for African Gospel music fans. Offering the latest news and information about Local and International Gospel music and news, Gospel in Africa Blog also shares the spotlight with other genres of Christian music that more than ever, seemingly overlap musical genre lines, such as Bluegrass Gospel, Christian Country and others. Singing News, the leading African Gospel and International music Blog, features African and international Gospel lyrics, radio, news, Christian concerts, songs, artists, and more.

GET IN TOUCH AND STAY CONNECTED WITH JOHN SHABANI

If you are interested in contacting and staying in touch with John Shabani then here are the contacts. E- mail: touchingvoice@yahoo.com or , princejohntz@yahoo.com, Mob: +255 754 818 767 or +255 716 560 094, www.facebook.com/john.shabani.

25 November 2019

WIMBO NI NINI?

Wimbo ni aina ya sanaa katika Fasihi ambayo hutumia lugha teule,sauti na kiimbo maalum. Nyimbo nyingi hugawanywa katika beti(verse) na kiitikio(chorus),pia zipo zenye kuwa na daraja/kiunganishi(bridge) na kiopoo/ndoano(hook). Pia nyimbo hutumia Ala za muziki kama vile ngoma,filimbi, gitaa na kinanda.
Ikumbukwe kuwa nyimbo zinaweza kuimbwa na mtu mmoja au zaidi.
SIFA ZA NYIMBO
1. Hutumia kiimbo au sauti maalum.
2. Huweza kuendana na Ala za muziki.
3. Huimbwa na mtu au watu kwa pamoja au kwa kupokezana.
4. Hutumia lugha ya mkato.
5. Hurudiarudia maneno ili kusisitiza ujumbe katika wimbo.
UMUHIMU WA NYIMBO
1. KUBURUDISHA.
2. KUELIMISHA, KUFUNZA, KUONYA NA KUELEKEZA, KULIWAZA, KUSIFIA KITU AU MTU KATIKA JAMII, KUUNGANISHA JAMII AU WATU TOFAUTI, KUDUMISHA/KUHIFADHI TAMADUNI ZA JAMII, KUKUZA TALANTA NA SANAA KATIKA JAMII, HUTUMIKA KATIKA MBINU ZINGINE ZA FASIHI KAMA VILE HADITHI MWISHO NYIMBO HUTUMIKA ILI KUMTUKUZA MUNGU MUUMBAJI.
Kabla sijaanza kutoa dondoo na maelezo ya namna au jinsi ya kuandika wimbo/uandishi,ni bora ukapata kujua baadhi ya mambo kuhusu nyimbo zenyewe na muziki kwa ujumla.

SONG STRUCTURE/MUUNDO WA WIMBO.
Ifahamike kwamba miundo ya nyimbo ipo mingi ikitegemea matakwa ya msanii au waandaaji wa wimbo husika.
MUUNDO WA NYIMBO ni mpangilio wa viunda wimbo katika mfutatano wa kujirudia. Hapa naongelea
1. ITRODUCTION/ITRO/MWANZO/UTAMBULISHO/UINGIAJI
2. KIITIKIO/CHORUS
3.VERSES/BETI
4.UTOKAJI/OUTRO/UMALIZIAJI/ENDING.
Viunda wimbo hivi hupangiliwa kulingana msanii anataka wimbo wake upangiliwe vipi. Ifuatayo ni mipangilio miwili pendwa na bora kutumiwa,ambayo ni;
1. Intro-chorus-verse-chorus-verse- chorus-outro.
2. Intro-verse-chorus-verse-chorus-verse-chorus-outro.
INTRO NA OUTRO.
Intro ni mwanzo wa wimbo, ni sehemu fupi ya mwanzo wa wimbo ambayo mara nyingi huwa na mistari minne tu. Mara nyingi hakuna vionjo Vingi vya midundo ni sehemu iliyo poa. Hapa ni sehemu utaaamua wimbo wako uanze vipi.
Outro ni sehemu ya mwisho ya wimbo au mwisho ambapo pia utaamua wimbo wako uishie vipi,mara nyingi ni baada ya kiitikio/chorus kurudiwa kwa mara ya mwisho au baada tu ya ubeti/verse ya mwisho inategemea na maamuzi yako msanii.
VERSES/BETI
Hiki ni kifungu kimoja cha shairi ambacho kina uzani sawa kutokana mpangilio wa vina vyako. Unaweza kuwa na verse yenye mashairi ya kimapokeo/yanayofata sheria za uandishi au verse yenye mashairi huru/ya kisasa/yasiyofuata sheria ili mradi yalete maana.
Hii ni sehemu ambayo stori yote ya wimbo huelezewa ni hapa ambapo unatakiwa kudadavua kinagaubaga ujumbe wako ukiendana na chorus/kiitikio chako pamoja na jina la wimbo wako maana ndio hubeba taswira ya beti/verse zako.
Mistari 16(sixteen bars) hutengeneza verse moja katika nyimbo mbalimbali ila sana za HIPHOP. Unaweza kuwa na verse ya misatari 8(8/eight bars), 12 adi 32,48,40/fourty bars.
Nakushauri andika mistari 16. Na mistari 8 unapoona inatosheleza mahitaji yako.
Wakati ujao tukijaaliwa nitafundisha jinsi ya kuhesabu mistari kulingana na midundo/beats,vina(vya mwanzo,vya kati,vya mwisho),pamoja na chorus/kiitikio.
By Vocal Coacher John Shabani


Anaehitaji huduma hii ya kuandikiwa nyimbo,
mawasiliano yapo apo juu.

UANDISHI AU UTUNZI WA NYIMBO (SONG WRITING/COMPOSITION)

Ebu tuangalie misingi ya utunzi wa nyimbo

JE UNAWAJUA WATU MUHIMU KWENYE KWAYA, BENDI AU KWA MWIMBAJI BINAFSI?

Ili wimbo uweze kukamilika huwa unakuwa na vipengele kadhaa ndani yake.
-       Kuna maneno au mashahiri, au kwa lugha ya siku hizi ‘mistari’ na kwa kiingereza Lyrics.
Nyimbo inaweza kuandikwa na mtu mmoja au wawili au Zaidi, tunawaita kwa kimombo Song writers. Mwandishi wa nyimbo anayeweka maneno ya wimbo (lyrics) eitha kwa kwa maneno ya kawaida au kwa nota huitwa Lyricict
-       Mistari huhitaji kupewa sauti ya kuimbia, Melody. Na huyo anayebuni au kutengeneza melody huitwa Composer. Lakini kama mtu atatengeneza vyote nilivyotaja hapo juu, kwa ufupi anatambulika kama mwandishi wa nyimbo (songwriter)
-       Baada ya hapo hutengenezwa arrangement, au mpangilio wa muziki huo, nini kinakuja wapi, waimbaji waimbe vipi na kujumlisha kazi zote hizi unapata wimbo mmoja.

Kwa uzoefu wa bendi au kwaya zetu, mara nyingi, Lyrics huletwa na mtu mmoja, anaweza akaleta mistari yenye melody au akaleta mistari peke yake na kutaka msaada wa wanamuziki wenzie watafute melody. Kazi inafuata ya arrangement pia hufanywa kwa ushirikiano na hatimae kukapatikana wimbo ambao kwa utamaduni wetu huwa tunatangaza kuwa mtunzi ni yule aliyekuja na mistari.

Si kila mtu ana kipaji cha kutunga, japo hiyo ndio imani ya wengi kuwa kila anaejua kuimba hujua kutunga. Waimbaji wengi maarufu duniani waliimba nyimbo zilizotungwa na wengine, na halikadhalika si kila anaetunga anajua kuimba, watunzi hata wa mashahiri huwaachia watu wengine waghani mashahiri yao, mtunzi akilazimisha kuimba wakati hana kipaji hicho matokeo ni madudu tu na hali kadhalika muimbaji asiye na kipaji cha kutunga aking’ang’ania kutunga kipawa chake cha kuimba kinaweza kisionekane kutokana na utunzi kuwa hafifu.
Na hali kadhalika si kila mtu ni arranger, tatizo ni pale asiekuwa na kipaji anaamua kufanya hiyo kazi, kinachotoka hakieleweki kama kinakwenda au kinarudi. Hali hii ipo pia kwa waimbaji binafsi(solo artist), wanataka kujionyesha wanajua kila kitu au wanafanya kila kitu, haiwezekani. Kuna wakati unahitaji aina fulani za tungo kutuko kwa  watunzi wazuri, una hitaji mwalimu au mtu wa kukuongoza kuwa bora zaidi, lakini pia zaidi ya hilo, unamwitaji arranger. Kama wewe umebahatika kufanya kila kitu basi mshukuru Mungu kwa hilo.
Kama nilivyosema awali katika bendi arrangement huwa ni mchango wa mawazo, lakini ukifanya utafiti kidogo utagundua hata katika kazi inayoonekana ya kikundi kuna mtu au watu ndio wanaoongoza nini kipigwe wapi. Nichukulie mfano wa bendi zilizopita, katika kutaka kujua undani wa jambo hili, nilipata maelezo ya kina kutoka kwa mkongwe wa muziki wa dansi hapa nchini, ndugu yetu John Kitime. Yeye anasema “Katika bendi nilizopitia kama vile Orchestra Mambo Bado, Orchestra Makassy au Vijana Jazz enzi hizo kulikuwa na mtu ana sauti ya mwisho kuhusu arrangement”
Kupendwa kwa wimbo ni mkusanyiko wa haya niliyoyataja hapo juu. Nyimbo nyingi zinazopendwa sasa hazitachukua muda kusahaulika kutokana na kuwa na arrangement hafifu sana. Mfumo wa sasa wa waimbaji kujaza wimbo wote bila kuweko na hata nafasi ya vyombo kutamba ni aina moja ya arrangement, lakini kwa mtazamo wangu nyimbo hizi zitasahaulika katika kipindi kifupi.
Katika mfumo wa uajiri au utafutaji wa wanamuziki katika vikundi vyetu, umuhimu hutolewa kwa wapiga vyombo na waimbaji, nadra kusikia mtunzi anatafutwa na nadra zaidi kusikia anatafutwa arranger, hivyo huwa bahati tu akatokea arranger mzuri au mtunzi mzuri katika kwaya au bendi na si kutokana na mipangilio. Pia nawajua arrangers wengi ambao hata wao hawajui kuwa ni arrangers, hivyo ‘majembe’ kama hayo yakifukuzwa au kuhama kwaya au bendi, basi vikundi hivyo vinaanza kudorora, na si mara moja nimekuta hata kwaya/bendi zenyewe hazijui kwanini ghafla kuna ukame wa tungo nzuri, pengine yule msanii aliyeitwa mzigo, kwa kuwa hakuwa muimbaji mzuri alikuwa ndie arranger bora wa kikundi hicho!!!
Labda niseme kwa kifupi, arrangement ndio ule mpangilio wa kuamua nini kipigwe na kipigwe wapi. Muziki unasheria za msingi kama vile hesabu.2+2=4, si nne na nusu wala na robo, arranger anakuwa na kipaji cha kupanga nini na anaweza kukueleza kwa nini pale kipigwe kinanda na gitaa liwe kimya au pale vipigwe vyote na kwanini iwe hivyo.
Muziki wetu wa wa kwaya au waimbaji wa siku hizi wakiwamo pia wale wa Bongoflava, umetawaliwa na waimbaji kwani swala la utunzi wa muziki na arrangement (kunakotambuliwa kama kutengeneza beat), huachiwa ‘producer’. Ni wazi ukisikiliza mfululizo wa nyimbo zinazotoka kila siku ni wazi kuwa maproducer wachache sana wanakipaji cha kuarrange, utasikia vyombo vinalia katika wimbo bila kuwa na mpangilio wala sababu ya kuwepo, hapa utasikia filimbi, mara saksafon, mara rimba, mara gitaa. Ninapo yasema hayo, sijawasahau wale waongozaji wazuri au masoloist, ambao ni watu pekee tena wenye mchango wa pekee kwenye vikundi vyetu vya uimbaji. Hawa nao wakiondoka huachapengo kubwa sana.

ZANA ZA UTUNZI
Mtunzi au mwandishi wa nyimbo, popote alipo anashauriwa kuwa na zana muhimu kama; Kifaa chochote cha kurekodia, daftari au notebook na kalamu. Kwa dunia ya leo, ukiwa na simu yako ya mkononi au tablet inatosha. Kwa lugha nyingine tunasema; Ikiwa kweli unataka kuchukua uandishi au utuzi wako wako wa wimbo kwa umakini mkubwa, unapaswa kujenga tabiaya kubeba zana au vifaa vya utunzi/uandishi wa nyimbo popote ulipo. (If you want to take your songwriting seriously and create authentic music, you should do your best to carry songwriting materials with you everywhere).

UANDISHI WA WIMBO.
MWANZO BORA WA UANDISHI BORA WA WIMBO.
Ifahamike ya kwamba kuna aina nyingi za kuanza kuandika wimbo, ila njia MAKINI ni ya kuanza na MADA ambayo itakupa JINA/TITLE.
UMUHIMU WA JINA/TITLE/MADA.
1. Jina la wimbo ni moyo wa wimbo.
2. Jina huelezea wimbo mzima.
3. Jina/Mada itakuongoza vyema ktk kuandika mistari na kukufanya usiandike nje ya mada.
Unda au chagua jina ambalo ni fupi si zaidi ya maneno matano (5) ili iwe rahisi kukumbukwa na mashabiki hata iwe rahisi kuiomba redioni au kuisema kwa marafiki au washikaji zao. Juu ya hili unaweza fanya uchunguzi wa kupitia majina ya nyimbo mbalimbali ili uone ufupi wa majina ya nyimbo unavyokuwa na madhara chanya kwa mashabiki.
Endelea kufatilia hii kitu tafadhari,na uwape habari marifiki. Wakati ujao tutaangalia kuhusu INTRO, CHORUS, VERSE, CHORUS, VERSE, CHORUS, OUTRO

Ukitaka Huduma ya kuandikiwa au kutungiwa limbo mzuri wasiliana namimi mwalimu wak wa Sauti Afrika Masahriki.


Kocha John Shabani

HEART OF WORSHIP

HEART OF WORSHIP