21 May 2014
MTUMISHI CHRISTOPHER MWAKASEGE NDANI YA DALLAS - USA
12:42
No comments
Itakua ni semina ya baraka tele ambapo kikundi cha Kystaal kitakua kikishusha uwepo wa Mungu kupitia sifa. ni kuanzia tarehe 1May - 30 June, Karibu na karibisha wengine!
20 May 2014
JOHN SHABANI BRINGS YOU JJ BARBER SHOP
05:47
No comments
Hey Dar es salaam, get ready for your Christian Barber shop;
by God's grace, it will be opening soon
"God bless T.B Joshua! God bless Bishop T.D Jakes"
You and others are really servants of God; that why I'm not ashamed of using your pictures
(Romes 1:16 For I am not ashamed of the gospel, because it is the power of God that brings salvation to everyone who believes: first to the Jew, then to the Gentile).
(Romes 1:16 For I am not ashamed of the gospel, because it is the power of God that brings salvation to everyone who believes: first to the Jew, then to the Gentile).
ALIYEKUWA ASKOFU MKUU WA MALAWI ASSEMBLIES OF GOD NI MMOJA KATI YA WAGOMBEA WA URAIS WA MALAWI
00:44
No comments
Kwa habari zaidi kuhusiana na mtumishi huyo wa Mungu aliye amua kujikita katika siasa, huku akiwa na ndoto nyingi za kuwa rais wa malawi, tembelea tofuti yake: www.chakwera.com
Leo Taifa la
malawi linapiga kura kuchagua Rais wa Taifa hilo kwa awamu nyingine...moja kati
ya wagombea ni Dr Lazarus Chakwera
ameingia kwenye siasa akitokea kuwa Askofu Mkuu wa Malawi Assemblies of
God(MAG),Mwenyekiti wa Assemblies of God Africa,Mwenyekiti wa Board wa All
Nations Theological Seminary...n.k;Nimependa ujasiri wake wa sio tu kusemea
madhabahuni au kwa waumini wake kimya kimya akaamua kujitosa na kutengeneza
mfano kwa vitendo,sijui kama atashinda ila naamini akishinda atakuwa mfano wa
kuigwa kwa maraisi wa Africa,he is a leader and Africa tuna tatizo la
viongozi,wanasiasa tunao wengi tu....
19 May 2014
UJUMBE MZITO KUTOKA KWA GAMA DANIEL MWASUMBI
11:01
No comments
Huyu hapa ni Gama Daniel Mwasumbi,
mtoto wa kiume wa Mch. Daniel Mwasumbi
Picha ya Mch. Mwasumbi katika cover ya video yake
ijulikanayo kwa jina la mkuyu uliokauka
Ikiwa ni takriban miezi 10 tangu kipenzi cha wengi na mkongwe wa muziki wa injili Tanzania, Mch. Daniel Mwasumbi kuhukumiwa kifungo jela, hapo chini ni ujumbe mzito alioandika rafiki yetu Gama Mwasumbi (Mtoto wa Mchungaji Mwasumbi):
“PESA unauwezo mkubwa sana wakufanya mema na Mabaya
kwa wakati mmoja.PESA unauwezo mkubwa sana wa kupenya hata kule ambako
kibinadamu inaonekana ngumu.Nimekuona ukifanya kazi Mahakamani, Hospitalini,
hata Makanisani.Una uwezo mkubwa sana wa kupindisha ukweli na ukaufanya Uongo
uonekane Mwema.Watu wameuwa, wametapeli, wamefanya uasi wa Ajabu lakini PESA
ukawahifadhi.
Asilimia kubwa mara nyingi asiyekuwa na wewe hana HAKI.
Nimeadhimia kukutafuta wewe Bwana Mkubwa PESA na nimeadhimia kwa Nguvu zote na akili zote ntakupata, kwasababu wewe ni Jibu la mambo yote.
Forgive me my Father if I had Money usingekuwa unateseka Jela mpaka sasa I tried tried to get you out of there, for something you didn't do it, lakini wale wenye PESA zao waliokuweka hapo bado wanaona ni vyema uendelee kuwepo hapo ndani.
I MISS YOU PAPS”!
Asilimia kubwa mara nyingi asiyekuwa na wewe hana HAKI.
Nimeadhimia kukutafuta wewe Bwana Mkubwa PESA na nimeadhimia kwa Nguvu zote na akili zote ntakupata, kwasababu wewe ni Jibu la mambo yote.
Forgive me my Father if I had Money usingekuwa unateseka Jela mpaka sasa I tried tried to get you out of there, for something you didn't do it, lakini wale wenye PESA zao waliokuweka hapo bado wanaona ni vyema uendelee kuwepo hapo ndani.
I MISS YOU PAPS”!
Kila unapopatapiga magoti kumwomba Mungu,
basi ikumbuke pia familia hii!
17 May 2014
TEMBELEA BLOGU MBALIMBALI ZA KIKRISTO TANZANIA
11:33
No comments
TEMBELEA BLOGU MBALIMBALI ZA KIKRISTO TANZANIA
Hizi ni baadhi ya blogu za kikristo Tanzania: Kwa habari za watumishi, huduma mbalimbali, matamasha, matukio mbalimbali,habari za kitaifa na kimataifa tembelea!
Kama wakristo na jamii kwa ujumla, kupata habari
mbalimbali nimuhimu sana. Baada ya rafiki zangu na wapenzi wa blogu yangu wa
ndani na nnje ya nchi kunitaka niweke orodha ya blogu za kikristo Tanzania,
basi imebidi nijaribu kutembelea blogu mbalimbali na kuzipata chache zenye
zisizo hegemea dini fulani na zenye mashiko. Najua zipo blog nyingi za kikristo, lakini pia
unaweza kunisaidia kuzifahamu pia. Hapa chini ni chache kati ya nyingi:8 May 2014
Michelle Obama aunga mkono kampeni ya kuwarudisha wanafunzi wa kike waliotekwa huko Nigeria – “Bring back our girls”
23:03
No comments
Michelle Obama akiwa ameshikilia bango akiungana na dunia katika kampeni ya kuwarudisha wanafunzi waliotekwa huko Nigeria
Mamia ya watu nnje ya ubalozi wa Nigeria huko Marekani, wakilalamikia serikali kutokuongeza bidii katika kuhakikisha wanafunzi wa kike waliotekwa wamerudishwa salama
Moja ya kati
ya habari kubwa dunia, ni ile ya kutekwa kwa wanafunzi huko Nigeria baada shule
ya mabweni ya wasichana kushambuliwa katika jimbo la Borno Kaskazini Mashariki
mwa nchi hiyo huku wasichana wakitekwa nyara.
Wazazi
wanasema kuwa zaidi ya wasichana miambili wametekwa nyara na washambuliaji hao. Kampeni hiyo ikiambatana na maandamano imefanyika karibu nchi mbalimbali duniani.
Taarifa zinazohusiana
Washambuliaji
wanaaminika kuwa wanachama wa kundi la wapiganaji wa kiisilamu la Boko Haram.
Utekaji nyara huo ulifanyika usiku wa manane katika shule ya Chibok Kusini mwa
mji wa Borno , karibu na mpaka na Cameroon.
Inaarifiwa
wasichana 300 walikuwa wanajiandaa kwa mitihani yao. Mmoja wa wasichana
alifanikiwa kutoroka na aliambia BBC kuwa walikuwa wanalala wakati walipovamiwa
na wanaume waliokuwa wamejihami.
Waliowashambulia
wanaaminika kuwa wapiganaji wa kundi la Boko Haram.
Wanaume
hao waliingiza magunia ya chakula katika malori yaona kuwaamuru wasichana
kupanda lori hizo.
Wasichana
15 walifanikiwa kutoroka baada ya lori walimokuwa kukumbwa na hitilafu.
Wakazi wa
kijiji cha Chibok wanasema kuwa walisikia milipuko kadhaa huku nyumba 170
zikiteketezwa.
Vyombo
vya habari nchini humo vimeripoti kuwa wanajeshi wawili waliuawa huku mali
ikiharibiwa wakati wa shamblizi hilo mjini Chibok.
Ni wito
wetu kuunga mkono kampeni hii na zaidi kumuomba Mungu ayanusuru maisha ya
wanafuzi hao.
Mungu
ibariki Nigeria,
Mungu ibariki Afrika,
Mungu inusuru Dunia na matukio ya
kutisha!
Subscribe to:
Posts (Atom)
HEART OF WORSHIP































