20 June 2014
MWIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI DEBORA SAID AFARIKI DUNIA
12:45
No comments
Mama Askofu, mwimbaji wa injili na mjumbe wa chama cha muziki wa injili, debora John Said hatunaye tena kimwili!...
Gospel in Africa imepokea kwa masikitiko makubwa sana juu ya
kifo cha Debora, tunawapa pole wafiwa na Watanzania wote na kupotelewa na
mtumishi wa Mungu na kipenzi cha wengi, mama Askofu John Said, mwimbaji na
mjumbe wa chama cha muziki wa Injili Tanznzania, ambaye amefanya kazi yake kwa
upendo na uaminifu. Mungu azidi kuipigania familia na wale wote waliokuwa wakimtegemea kiroho na
kimwili. Ni wakati wa waimbaji wa nyimbo za injili kujifunza jambo, kurudiaha umoja
na upendo aliotuachia Yesu. Sisi tuliobaki tuzidi kumtumikia Mungu kwani
hatujui vilivyombele yetu.
Huu ni wakati wa kuungama na kutubu makosa
tunayoyafanya katika maisha yetu hapa duniani. Mungu amekupa kipaji fulani kwa
kazi yake basi kitumia na usiache. Debora amefanya kazi ya Mungu kwa njia ya
uimbaji kwa umaminifu mwingi, bila skendo, bila majivuno wala majigambo,
amekuwa ni mshauri mzuri, hakuwa na wivu kabisa, na sasa ametangulia.
IBADA YA KUMUAGA ITAFANYIKA JUMATATU SAA NNE ASUBUHI KATIKA
KANISA LA MAISHA YA USHINDI MABIBO EXTERNAL NA BAADAYE SAA NANE MCHANA MAZISHI
KATIKA MAKABURI YA MABIBO JESHINI.
John
Shabani
Katibu
chama cha muziki wa injili Tanzania
17 June 2014
CHAMA CHA MUZIKI WA INJILI TANZANIA KUKULETEA MBEYA GOSPEL FESTIVAL
15:33
No comments
Hawa ni wachache kati ya wengi watakaomtumikia Mungu kwa njia ya uimbaji, maigizo pamoja na neno la Mungu siku hiyo.
Uongozi wa Chama cha muziki wa Injili Tanzania unawakaribisha wakaaji wote wa mbeya na maeneo ya jirani, kuja kubarikiwa na waimbaji mbalimbali wa injili kutoka mikoa mbalimbali. Lengo likiwa kwanza ni kumtumikia Mungu, kuhamasisha watu kujiunga na chama ili kudumisha umoja wetu; Kumbuka umoja ni nguvu.
Karibuni sana.
MUME MWEMA NI YUPI?
07:37
No comments
Ni maswali ambayo majibu yake yana utata mwingi, wengine wakidhani kuwa wamepata mwisho wa siku ni majuto, na wengine wakionekana kuwa ndivyo sivyo kumbe wamepatia...
Mume mwema hatoki kwa ATM ao sio awe kama ATM eti ndo mume mwema , mume mwema sio muonekano ao kuwa anamilika nyumba, magari, kazi ya juu, ao kabila . Tumeshuhudia mara nyingi watu walikimbilia kuolewa na masupasta, matajiri au vijana watanashati lakini mwisho wake ni vilio, na wengine kupelekana kaburini. Sijapinga suala la kuwa na chagua la aina ya mwenzi unayemtaka, lakini Mungu apewe nafasi ya kwanza katika maamuzi
Ebu angalia picha hii jinsi wanavyopendeza.
Swali langu ni hili:
Hivi unapoomba Mungu akupe mume mwema, una maanisha nini?
Je ni mume ambaye anajali familia pia ana upendo kwa familia yake? Ni
msomi, mwenye kipato kizuri, mtanashati au aliyeshikilia dini sana au mtu wa
sala? . Mungu anajibu maombi kwa aina nyingi sana lakini wanadamu huwa
tunapingana na mpango wa mungu
Mume mwema hatoki kwa ATM ao sio awe kama ATM eti ndo mume mwema , mume mwema sio muonekano ao kuwa anamilika nyumba, magari, kazi ya juu, ao kabila . Tumeshuhudia mara nyingi watu walikimbilia kuolewa na masupasta, matajiri au vijana watanashati lakini mwisho wake ni vilio, na wengine kupelekana kaburini. Sijapinga suala la kuwa na chagua la aina ya mwenzi unayemtaka, lakini Mungu apewe nafasi ya kwanza katika maamuzi
Ebu angalia picha hii jinsi wanavyopendeza.
kila mtu vyovyote vile alivyo
anaweza kuwa mume mwema!...
15 June 2014
ON FATHER’S DAY MWANZILISHI WA KANISA LA T.A.G MAGOMENI AMEKABIDHIWA ZAWADI YA GARI
22:29
No comments
Hapa Mch. Sasali akijiandaa kukata utepe wa zawadi ya Gari alilokabidhiwa na kanisa la T.A.G Magomeni
Hilo hapo gari lenyewe
Sasali family: Mch. Sasali, Mch. Matthew Sasali,
Happy Sasali, Mama yetu, Samuel Sasali na Joel Sasali
Natanguliza ujumbe huu kutoka ukura wa facebook wa Sam Sasali:
“On Father's Day Dad and Mum wamepokea zawadi ya Toyota
Xtrail kutoka kwa Kanisa la Magomeni TAG Magomeni Kama Ishara ya Kutambua Ubaba
wake. Happy Fazas Day. God bless u Pastor Dunstan Kanemba. Happy Birthday”.
Ninachoweza kukisema ni kama vile ambavyo wengine wameshasem;
Katika vitu ambavyo vimenibariki leo ni kupata taarifa ya habari njema sana
kwangu kwamba Mch. Sasali (Sr.) amepewa zawadi ya gari 4WD na kanisa ambalo
amelilea sana kwa miaka mingi, Magomeni TAG. Nakumbuka Miaka kadhaa iliyopita
nikiwa mwalimu wa kwaya na shemasi katika kanisa la T.A.G Mwanga Kwa Askofu
Mulenda Omary, Kati ya watumishi walinibariki sana ni Mch. Nathaniel Sasali,
kipindi hicho akiwa mwinjilisti wa kitaifa wa Tanzania Assemblies Of God.
Nilijikuta nikiwa na Spiritual connection na mtumishi huyo; na baada ya muda
mfupi nilijielekeza Dar na ghafla nikawa mwalimu wa kwaya ya hapohapo magomeni
T.A.G
Moja ya watumishi walionifanya niwe hivi nilivyo na
nitakavyokua, ni Mzee Nathanieli Sasali. Kuna kitu kizuri sana pale
tunapotambua michango ya wachungaji na watumishi wa Mungu ambao ni genuine, katika
ujana wao na utu uzima wao, hawa wazee wamekuwa wanamtumikia Mungu sio kwa
sababu "huduma inalipa" ila kwa sababu wana wito.
Ahsanteni sana Magomeni TAG, kwa kutambua mchango wa Baba!
12 June 2014
WAIMBAJI WA INJILI WALIOOA NA KUOLEWA
03:16
No comments
Mr & Mrs John Lisu
Jojo Jose & Matilda
Stella Joel & husband
Mr & Mrs David Robert
Mr &Mrs Addo November
Mr & Mrs Joshua Makondeko
Mr & Mrs Jangalason
Jesca BM & Husband
Mr & Mrs Bony Mwaitege
Upendo Nkone & Husband
Mr & Mrs Victor Aron
Nimeweka
habari hii baada ya kuambiwa mara nyingi eti karibu waimbaji wengi wa injili
Tanzania hawajaoa au kuolewa, mimi nasema si kweli, kwa kuthibitisha hilo hawa
hapa chini ni baadhi ya waimbaji wachache kati ya wengi wenye ndoa zao.
Kuoa ni
mpango kamili wa Mungu, hivyo wenzangu namimi foleni hii imesogea sasa ebu
tuingie katika taasisi hii ili kutimiza haki yote na pia kujihepusha na maswali
yasiyokuwa na sababu…
Kwa wale
nilioweka picha zao, samahani kama nimemkwaza mtu, hasa kwa wale wasiotaka
kujulikana kwamba ameoa au kuolewa, lakini pia picha hizi sijazipata mbinguni,
ni humuhumu mtandaoni
Mungu awabariki wana
ndoa
Mungu wasaidie wale
ambao bado
Amen!
9 June 2014
WAJANE WATOKWA NA MACHOZI YA FURAHA BAADA HUDUMA YA RLM KUWAKUMBUKA
06:48
No comments
Mtumishi wa Mungu, Mary Lutumba akitoa zawadi ya upendo kwa wajane
Mtumishi David Lutumba akiwatia moyo kina mama hao baada ya kuwapa pesa za kujikimu ki maisha
Mama akitokwa na machozi ya furaha
Ni katika semina kubwa iliyoandaliwa na huduma ya River of Life – Mlima
wa mabadiliko ikiongozwa na watumishi wa Mungu, Mary na David Lutumba. Ujumbe
wa semina ulikua:
“KUKOMESHA MSIBA WA MWANAMKE”
(marko 5:34)Wanawake na kinamama wengi
wamefunguliwa katika semina hiyo.
Kama ilivyo kawaida ya blogu hii yenye wapenzi wengi duniani, lengo letu ni kutangaza huduma mbalimbali, tutaendelea kukujulisha mengi zaidi kuhusu huduma hiyo na wapi wanapatikana, endelea kufuatilia hapahapa!...
Subscribe to:
Posts (Atom)
HEART OF WORSHIP











































