THE OFFICIAL JOHN SHABANI AND GOSPEL IN AFRICA BLOG

Welcome to the official blog of the the gospel singer, songwriter and teacher John Shabani. If you are one of the fans among the millions, feel free to get connected with John Shabani and stay updated on this blog.To learn more about John Shaban and his Ministry, please click the about button above.

GET THE LATEST FROM JOHN SHABAN AND THE GOSPEL NEWS COMMUNITY

You will be able to read and review the latest news on John Shabani's tour and other specials. You will also come across the best articles of news on Gospel from all across Africa and the International Community.Please do feel free to review our categories of news and events.

FEEL FREE TO LEARN MORE ABOUT JOHN SHABANI AND HIS MINISTRY

If you wish to learn more about John Shabani and his ministry, please feel free to connect with John Shabani on the social networks. You can keep up with John Shabani and the Gospel in Africa community on both twitter, facebook, google plus and many other more.

STAY UPDATED WITH INTERNATIONAL AND LOCAL GOSPEL NEWS

Gospel in Africa Blog is a comprehensive gathering place for African Gospel music fans. Offering the latest news and information about Local and International Gospel music and news, Gospel in Africa Blog also shares the spotlight with other genres of Christian music that more than ever, seemingly overlap musical genre lines, such as Bluegrass Gospel, Christian Country and others. Singing News, the leading African Gospel and International music Blog, features African and international Gospel lyrics, radio, news, Christian concerts, songs, artists, and more.

GET IN TOUCH AND STAY CONNECTED WITH JOHN SHABANI

If you are interested in contacting and staying in touch with John Shabani then here are the contacts. E- mail: touchingvoice@yahoo.com or , princejohntz@yahoo.com, Mob: +255 754 818 767 or +255 716 560 094, www.facebook.com/john.shabani.

20 November 2014

CHAMA CHA MUZIKI WA INJILI TANZANIA NA MKAKATI WA KUPANDA MITI NA MICHE YA MATUNDA NA MAUA NCHI NZIMA



Hii ni ziara ya kihistoria iliyoandaliwa na chama cha Muziki wa Injili Tanzania.

Mungu alipoumba Dunia, aliifanya yenye kupendeza na kuvutia sana, lakini kwasababu ya matumizi mabaya ya wanadamu, sasa maeneo mengi duniani yanaonekana kama jangwa, kwasababu ya matumizi mabaya ya ardhi, kumekuwa na ukame uliokithiri, ardhi sasa haina rutba ya asili, joto linasumbua duniani kote, majira ya upatikanaji mvua yamebadilika sana; wanaoathirika ni viumbe hai akiwemo mwanadamu.
Kwakulitambua hilo, waimbaji wa nyimbo za injili, tumeamua kujitolea kufanya kampeni nchi nzima ya upandaji miti pamoja na miche ya maua na matunda ili kurejesha uoto wa asili katika nchi yetu.
Pamoja na hayo pia ziara hiyo inaandaa matamasha ya uimbaji ikiwa ni pamoja na kuwahubiri watu waache uovu na kuishi maisha ya kumpendeza Mungu. Jambo linguine la msingi ni pamoja na kuwa na kuiombea nchi  amani, utulivu, umoja na mshikano wetu.
Baada ya ziara ya umisheni mkoani singida, waimbaji walipata fursa ya kuhudhuria kikao cha bunge na baadaye kupata picha ya pamoja na  Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda, Naibu Waziri wa Fedha Mh. Mwigulu Nchemba, Waziri wa Maliasili na Utalii Mh. Razaro Nyarandu, Mbunge wa CCM Viti Maalum – Singida Mh. Martha Mlata, Mbunge wa Viti Maalum CCM – Mbeya Mh. Marry Mwanjelwa, Mh. Magreth Sitta na wengine wengi.
Ziara ilihitimishwa kwa kupata chakula cha mchana kilichoandaliwa na Mh. Nyarando ndani ya Dodoma Hotel. Mh. Nyarando aliweza kuwashukuru waimbaji kwa ushiriakiano wao na jinsi walivyoweza kujitolea kufika vijijini kufanya kazi ya Mungu.
Pia aliweza kuwaahidi waimbaji kutembelea Ngorongoro Crater mapema iwezekanavyo, ili kujifunza mambo mengi ikiwa ni pamoja na kutangaza vivutio vya utalii.

Kwa msaada wa Mungu tunaweza!

 waimbaji wakiwa wamejipanga tayari kuelekea kupanda miti


 Msafara wa waimbaji wakishirikiana na wanakijiji wa tarafa ya Ndago mkoani Singida pamoja na viongozi wa dini, wakielekea kupanda miti
 Mheshimiwa Martha Mlata akipanda mti
  Stela Joell akipanda mti
  Madam Ruti akishirikiana na mtangazaji wa Star Tv, bi Sauda  kupanda mti
 John shabani na Jane Misso, wakipanda mti
 Edson Mwasabwite akipanda mti
Mch. Vaileth na Bupe kingu wakishirikiana na watumishi wengine kupanda mti

4 November 2014

Mafundisho ya Askofu Kakobe Kuhusu Pete – asema pete ya ndoa si mpango wa Mungu!



Ni maelezo mbalimbali kuhusu maisha ya Akofu. Baada ya kuulizwa maswali mbalimbali kuhusu maisha yake na huduma, hapa Askofu Zakaria anaendelea kumjibu mwandishi:

Naendelea kuwaletea maelezo kuhusu maisha ya Askofu Kakobe baada ya kuokoka na kuanzisha kanisa.

Mwandishi: Kuna waliosema kuwa ulianzisha kanisa nchini Marekani na ulikuwa na mpango wa kuhamia huko, je ni kweli?

Askofu Kakobe: Kuhama nchi siwezi lakini ni kweli baada ya maombi ya muda mrefu Aprili 16, 2012 nilifungua kanisa Marekani, hii ni nia ileile ya kuokoa mataifa na kuinua jina la Yesu.

Mwandishi: Tunaona watu wakifunga ndoa wanavaa pete lakini katika kanisa lako hilo halipo, unazungumziaje hilo?

Askofu Kakobe: Pete kwenye ndoa siyo agizo la Bwana na ndiyo maana tunaona Mungu mwenyewe akichukizwa na watu waliovaa pete, vikuku na mapambo mengineyo. Soma maandiko haya Isaya 3:21, 16-24; Hosea 2:13;  Mwanzo35:1-5; Kutoka 33:4-6; Yeremia 4:30; 1Timotheo 2:9-10; 1Petro 3:3-5. Mapambo ni mavazi ya waabudu miungu, yanahusishwa na ibada ya miungu (mashetani).

Mwandishi: Lakini wanaotumia pete katika ndoa wanasema eti pete ni mfano wa upendo usio na mwanzo na mwisho, unasemaje kuhusu madai hayo?
Askofu Kakobe: Hiyo siyo kweli, mwanzo wa upendo ni pale walipokutana na wakapendana na mwisho wa upendo ni pale mmoja  anapofariki na kumfanya mwenzake kuwa huru kuolewa au kuoa. Yesu alisema mbinguni hakuna kuoa wala kuolewa.

Hutapewa mke wako au mume wako uishi naye huko mbinguni. Yote hii ni janjajanja ya shetani anayekuja kwa mfano wa malaika wa nuru ili kutufanya tuingize mapambo katika nyumba ya Mungu na kujenga ngome za mashetani kwa visingizio  kwamba mimi nimevaa pete sasa ni mke wa mtu au mume wa mtu. Mbona nyumba za wageni (guest houses) zimejaa watu wenye pete za ndoa? Kama pete hizo zingekuwa zinawafanya watu wasiwe makahaba, tusingekuwa na matatizo tuliyonayo leo.

Habari kutoka: www.kigoma24hours.blogspot.com


30 October 2014

MKAKATI WA KUWASAIDIA WATOTO YATIMA



 Bi Warra Nnko akiwa amekumbatia kitoto kichanga kilicholetwa baada ya mama yake kufariki wakati wa kujifungua

 Baadhi ya watoto wakipata kifungua kinywa



 Muonekano wa jengo la Shalom Orphanage Center

 John shabani akitoa mafunzo kwa watoto




 Mwenyekiti wa Chama Cha Wajane Tanzania, akiwa katika hali ya huzuni baada ya kujionea hali mbaya ya baadhi ya watoto walioletwa katika kituo cha Shalom

Hawa ni watoto wanaolelewa katika kituo cha SHALOM! watoto hawa, waliookotwa vichakani hali zao zikiwa mbaya sana, kila mara baba yao mzazi ambaye ni mlevi wa kupindukia, aliwalawiti kwa zamu. Maisha yao yalikua ya kuokota vyakula vilivyotupwa jalalani, huku makazi yao yakiwa ni kulala vichakani baada ya nyumba yao ya majani kuanguka.

 Watoto wakisherekea sikukuu ya Christsmass

 Wageni mbalimbali hujitolea kufanya kazi za kijamii katika kituo


 Moja ya madarasa

Baada ya kuzunguka maeneo mbalimba, hii ni ziara nyingine ya kutembelea kituo cha watoto yatima
                              “SHALOM ORPHANAGE CENTER”!    
                                           Mimi na wewe tunaweza.

Jambo moja nililojifunza chini ya jua, ni kufanya Jambo sahihi, kwa mazingira sahihi, kwa watu sahihi, na kwa wakati sahihi. Jambo lako, wazo lako, uamuzi wako, mkakati wako vyaweza kuwa, sahihi lakini si kwa watu sahihi, labda si kwa mazingira sahihi, lakini pia labda si kwa wakati sahihi.
Inawezekana umekuwa ukifanya mambo mengi, lakini pia unataka uonekane na watu, upongezwe au uambiwe asante! Si vibaya, lakini wakati mwingine fanya jambo katika mazingira ambayo si ya kupongezwa wala kusifiwa bali kwako ni wajibu kama mwanadamu ambaye uhai wako hujaugharimia chochote.

Moja ya mambo nilioamua ni kuwaona watu wenye uhitaji haswa tena huko maeneo ya vijijini, hilo ni jukumu letu sote. Ndio maana baada ya kuzungukia vituo mbalimba vya watoto yatima Tanzania, ziara iliyoratibiwa na Chama cha Wajane Tanzania (Tanzania Widows Association), moja ya kituo kilichonigusa sana ni cha SHALOM ORPHANAGE CENTER, kilichopo huko karatu, kilomita 160 kutoka jiji la Arusha. 

Moja ya vitu nilivyoguswa navyo ni kumuona mama mjane Bi Warra Nnko, akiwa amegeuza nyumba yake kuwa kituo cha kulelea watoto. Vipo vyumba vya watoto wachanga haswa, wengine wameokotwa wakiwa wametupwa baada ya kuzaliwa na wengine wazazi kufariki wakati wa kujifungua. Pia wapo watoto ambao huletwa wakiwa katika hali mbaya, wangine wamebakwa na kulawitiwa. Nilitiwa moyo kuona hata serikali ya wilaya na hata mkoa huleta watoto katika kituo hicho. 

Vipo vyumba vya watoto wenye hali mbaya, wengine wanaulemavu wa aina mbalimbali, wengine wameathiki na ukimwi n.k. Shalom Orphanage center ni kama Hospital, Shule, na mji wa makimbilio. Pia nimeguswa kuona Bibi huyo ameanzisha miradi mbalimbali ikiwemo ya ng’ombe wa maziwa, kuku wa mayai na mashamba ili watoto wapate lishe na afya bora. Ukifika shalom lazima ulie kidogo; lakini cha kushangaza watoto hao,kuanzia wachanga na wale wanaosomeshwa sekondari wote humwita Bibi Warra Mama!

Mimi kama mwalimu wa sauti na uimbaji, nikiwanimeambatana na mwenyekiti wa Chama Cha Wajane Tanzania na baadhi ya watu, pamoja na kila mtu kutoa kile alichokuwanacho, lakini pia niliamua kuanzisha mpango wa kuibua vipaji vya watoto.

Wito wangu kwako, ni kukuomba tuungane kwa pamoja safari hii tena, kwa chochote ulichonacho tukawaone watoto hao mwishoni mwa mwezi huu wa Novemba. Pia ikumbukwe kuwa karatu nisehemu nzuri ya utalii wa ndani, utajifunza mengi pale MTO WA MMBU, lakini pia kutembelea mbuga za SERENGETI, NGORONGORO, pamoja na kutembelea kwenye misitu na mapango ya mawe wanakoishi waadzabe. 

Unaweza ukaleta nguo, chakula, pesa yako na chochote ulichonacho kisha ukakabidhi katika ofisi za Chama cha Wajane Tanzania zilizopo maeneo ya kinyerezi.
Kwa mawasiliano zaidi tupigie: 0754 366 530, 0713778778

14 October 2014

KUTUMIA NGUVU ILI KUIMBA VIZURI



Hapa ni mwalimu John Shabani sambamba na Masanja mkandamizaji pamoja na Emmanuel Mabisa wakimtumikia Mungu kwa njia ya uimbaji

Huu ni muendelezo wa masomo yanayofundishwa na John shabani, ili kukufanya unayetaka kujifunza kuimba, uwe mwanafunzi mzuri na yule mwimbaji awe bora zaidi.

Tahadhari: Usilazimishe kutumia nguvu ili uweze kuimba vizuri, kinyume chake jizoeshe kutumia nguvu kidogo lakini utaalam mwingi (Vocal Technique). Shida ni pale tunapodhani kwamba nguvu hizi ni kama za wanariadha au wacheza mieleka! Inawezekana nguvu hizi zisionekane kwa macho ya nyama lakini zinadhihirishwa na uimbaji wetu. Tunapoimba tunatakiwa kuwa na uhuru (freedom in singing), na sio kama mtu aliyelazimishwa. Lakini ikumbukwe pia nguvu hizi asili yake inatoka pia na mfumo wetu wa maisha ya kila siku iki pia ni pamoja na mazoezi ya viungo, vyakula na vinyaji tunavyotumia, makazi na malazi safi n.k.
Mazoezi mengi yanayofanyika kwenye vikundi mbalimbali, ni ya kupayuka na kutumia nguvu nyingi, matokeo yake watu wengi wamekaa kwenye zoezi hilo kwa muda mrefu bila kuwa na mabadiliko yoyote huku miili yao ikizoofika au kuishia kuwa mtu wa kupiga kelele na sio kujfunza kuimba vizuri. Haya sio mazoezi ya kumpata mshindi wa dansi mia mia, ni mazoezi ya kuimba. Imefika mahali sasa masikio hayawezi kujisikia vile tunavyoimba kwasababu ni kelele na kujichosha.
Ikumbukwe kuwa sauti hutunzwa kama yai; wengi wetu hufanyishwa mazoezi magumu yasiyolingana na umri wao na hali yao ya mfumo wa miili yao pamoja na kuzingatia afya zao, matokeo yake nimeshuhudia watu wakipata matatizo katika koo zao na hata bathi ya miili yao. 

Inashangaza kuona mtu ambaye hajawahi kukimbia maili moja unataka kumkimbiza maili kumi, matokeo yake ni kudondoka kama sio kupoteza fahamu kabisa. Yapo mazoezi ya kawaida ya jumla lakini mazoezi mengine ya uimbaji lazima yazingatie umri wa mtu, hali ya mtu huyo sambamba na afya yake. Nasikitika kusema kuwa wapo waliofundishwa kwamba akiweza kuimba noti za juu ndio amekuwa mwimbaji mzuri, matokeo yake mtu anatumia nguvu nyingi, kukaza misuli ya uso huku usoni akijaribu kuvimba na kutoa macho kama mjusi aliyebanwa na mlango ili tu awezekufika huko!...

Najua wapo waalimu wengi katika masomo haya ya uimbaji, na wengine inategemea amejifunza wapi, lakini bado mwisho wa siku ukweli unabaki kuwa ukweli. Mimi ningeshauri hata kama wewe ni mwalimu mzuri, mwimbaji mzuri, sote tubaki kuwa wanafunzi.

Kwa ushauri zaidi tupigie
0716560094, au  niandikie: touchingvoice@yahoo.com
Pia unaweza ukahudhuria masomo tunayofundisha sehemu mbalimbali.

12 October 2014

John Shabani - Mtoto wa Mfalme

HEART OF WORSHIP

HEART OF WORSHIP