20 November 2014
CHAMA CHA MUZIKI WA INJILI TANZANIA NA MKAKATI WA KUPANDA MITI NA MICHE YA MATUNDA NA MAUA NCHI NZIMA
20:01
No comments
Hii ni ziara ya kihistoria
iliyoandaliwa na chama cha Muziki wa Injili Tanzania.
Mungu alipoumba Dunia,
aliifanya yenye kupendeza na kuvutia sana, lakini kwasababu ya matumizi mabaya
ya wanadamu, sasa maeneo mengi duniani yanaonekana kama jangwa, kwasababu ya matumizi
mabaya ya ardhi, kumekuwa na ukame uliokithiri, ardhi sasa haina rutba ya
asili, joto linasumbua duniani kote, majira ya upatikanaji mvua yamebadilika
sana; wanaoathirika ni viumbe hai akiwemo mwanadamu.
Kwakulitambua hilo,
waimbaji wa nyimbo za injili, tumeamua kujitolea kufanya kampeni nchi nzima ya
upandaji miti pamoja na miche ya maua na matunda ili kurejesha uoto wa asili
katika nchi yetu.
Pamoja na hayo pia ziara
hiyo inaandaa matamasha ya uimbaji ikiwa ni pamoja na kuwahubiri watu waache
uovu na kuishi maisha ya kumpendeza Mungu. Jambo linguine la msingi ni pamoja
na kuwa na kuiombea nchi amani, utulivu,
umoja na mshikano wetu.
Baada ya ziara ya umisheni
mkoani singida, waimbaji walipata fursa ya kuhudhuria kikao cha bunge na
baadaye kupata picha ya pamoja na Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda, Naibu Waziri wa Fedha Mh. Mwigulu
Nchemba, Waziri wa Maliasili na Utalii Mh. Razaro Nyarandu, Mbunge wa CCM Viti
Maalum – Singida Mh. Martha Mlata, Mbunge wa Viti Maalum CCM – Mbeya Mh. Marry
Mwanjelwa, Mh. Magreth Sitta na wengine wengi.
Ziara
ilihitimishwa kwa kupata chakula cha mchana kilichoandaliwa na Mh. Nyarando
ndani ya Dodoma Hotel. Mh. Nyarando aliweza kuwashukuru waimbaji kwa
ushiriakiano wao na jinsi walivyoweza kujitolea kufika vijijini kufanya kazi ya
Mungu.
Pia aliweza
kuwaahidi waimbaji kutembelea Ngorongoro Crater mapema iwezekanavyo, ili
kujifunza mambo mengi ikiwa ni pamoja na kutangaza
vivutio vya utalii.
Kwa msaada wa Mungu
tunaweza!
waimbaji wakiwa wamejipanga tayari kuelekea kupanda miti
Msafara wa waimbaji wakishirikiana na wanakijiji wa tarafa ya Ndago mkoani Singida pamoja na viongozi wa dini, wakielekea kupanda miti
Mheshimiwa Martha Mlata akipanda mti
Stela Joell akipanda mti
Madam Ruti akishirikiana na mtangazaji wa Star Tv, bi Sauda kupanda mti
John shabani na Jane Misso, wakipanda mti
Edson Mwasabwite akipanda mti
Mch. Vaileth na Bupe kingu wakishirikiana na watumishi wengine kupanda mti
4 November 2014
Mafundisho ya Askofu Kakobe Kuhusu Pete – asema pete ya ndoa si mpango wa Mungu!
20:52
No comments
Ni maelezo mbalimbali kuhusu
maisha ya Akofu. Baada ya kuulizwa maswali mbalimbali kuhusu maisha yake
na huduma, hapa Askofu Zakaria anaendelea kumjibu mwandishi:
Naendelea kuwaletea maelezo kuhusu
maisha ya Askofu Kakobe baada ya kuokoka na kuanzisha kanisa.
Mwandishi: Kuna waliosema kuwa
ulianzisha kanisa nchini Marekani na ulikuwa na mpango wa kuhamia huko, je ni
kweli?
Askofu Kakobe:
Kuhama nchi siwezi lakini ni kweli baada ya maombi ya muda mrefu
Aprili 16, 2012 nilifungua kanisa Marekani, hii ni nia ileile ya kuokoa mataifa
na kuinua jina la Yesu.
Mwandishi: Tunaona watu wakifunga
ndoa
wanavaa pete
lakini katika kanisa lako hilo halipo, unazungumziaje hilo?
Askofu Kakobe: Pete kwenye ndoa
siyo agizo la Bwana na ndiyo maana tunaona Mungu mwenyewe
akichukizwa na watu waliovaa pete, vikuku na mapambo mengineyo. Soma maandiko
haya Isaya 3:21, 16-24; Hosea 2:13; Mwanzo35:1-5; Kutoka 33:4-6; Yeremia
4:30; 1Timotheo 2:9-10; 1Petro 3:3-5. Mapambo ni mavazi ya waabudu miungu,
yanahusishwa na ibada ya miungu (mashetani).
Mwandishi: Lakini wanaotumia pete
katika ndoa wanasema eti pete ni mfano wa upendo usio na mwanzo na mwisho,
unasemaje kuhusu madai hayo?
Askofu Kakobe: Hiyo siyo kweli,
mwanzo wa upendo ni pale walipokutana na wakapendana na mwisho wa upendo ni
pale mmoja anapofariki na kumfanya mwenzake kuwa huru kuolewa au kuoa.
Yesu alisema mbinguni hakuna kuoa wala kuolewa.
Hutapewa mke wako au mume wako
uishi naye huko mbinguni. Yote hii ni janjajanja ya shetani anayekuja kwa mfano
wa malaika wa nuru ili kutufanya tuingize mapambo katika nyumba ya Mungu na
kujenga ngome za mashetani kwa visingizio kwamba mimi nimevaa pete sasa
ni mke wa mtu au mume wa mtu. Mbona nyumba za wageni (guest houses) zimejaa
watu wenye pete za ndoa? Kama pete hizo zingekuwa zinawafanya watu wasiwe
makahaba, tusingekuwa na matatizo tuliyonayo leo.
Habari
kutoka: www.kigoma24hours.blogspot.com
30 October 2014
MKAKATI WA KUWASAIDIA WATOTO YATIMA
15:45
No comments
Bi Warra Nnko akiwa amekumbatia kitoto kichanga kilicholetwa baada ya mama yake kufariki wakati wa kujifungua
Baadhi ya watoto wakipata kifungua kinywa
Muonekano wa jengo la Shalom Orphanage Center
John shabani akitoa mafunzo kwa watoto
Mwenyekiti wa Chama Cha Wajane Tanzania, akiwa katika hali ya huzuni baada ya kujionea hali mbaya ya baadhi ya watoto walioletwa katika kituo cha Shalom
Hawa ni watoto wanaolelewa katika kituo cha SHALOM! watoto hawa, waliookotwa vichakani hali zao zikiwa mbaya sana, kila mara baba yao mzazi ambaye ni mlevi wa kupindukia, aliwalawiti kwa zamu. Maisha yao yalikua ya kuokota vyakula vilivyotupwa jalalani, huku makazi yao yakiwa ni kulala vichakani baada ya nyumba yao ya majani kuanguka.
Watoto wakisherekea sikukuu ya Christsmass
Wageni mbalimbali hujitolea kufanya kazi za kijamii katika kituo
Moja ya madarasa
Watoto wakisherekea sikukuu ya Christsmass
Wageni mbalimbali hujitolea kufanya kazi za kijamii katika kituo
Moja ya madarasa
Baada ya kuzunguka maeneo mbalimba, hii ni ziara nyingine
ya kutembelea kituo cha watoto yatima
“SHALOM ORPHANAGE
CENTER”!
Mimi na wewe tunaweza.
Jambo moja
nililojifunza chini ya jua, ni kufanya Jambo sahihi, kwa mazingira sahihi, kwa
watu sahihi, na kwa wakati sahihi. Jambo lako, wazo lako, uamuzi wako, mkakati
wako vyaweza kuwa, sahihi lakini si kwa watu sahihi, labda si kwa mazingira
sahihi, lakini pia labda si kwa wakati sahihi.
Inawezekana
umekuwa ukifanya mambo mengi, lakini pia unataka uonekane na watu, upongezwe au
uambiwe asante! Si vibaya, lakini wakati mwingine fanya jambo katika mazingira
ambayo si ya kupongezwa wala kusifiwa bali kwako ni wajibu kama mwanadamu
ambaye uhai wako hujaugharimia chochote.
Moja ya
mambo nilioamua ni kuwaona watu wenye uhitaji haswa tena huko maeneo ya vijijini,
hilo ni jukumu letu sote. Ndio maana baada ya kuzungukia vituo mbalimba vya
watoto yatima Tanzania, ziara iliyoratibiwa na Chama cha Wajane Tanzania (Tanzania Widows Association), moja ya
kituo kilichonigusa sana ni cha SHALOM ORPHANAGE CENTER, kilichopo huko karatu,
kilomita 160 kutoka jiji la Arusha.
Moja ya
vitu nilivyoguswa navyo ni kumuona mama mjane Bi Warra Nnko, akiwa amegeuza nyumba yake kuwa kituo cha kulelea
watoto. Vipo vyumba vya watoto wachanga haswa, wengine wameokotwa wakiwa
wametupwa baada ya kuzaliwa na wengine wazazi kufariki wakati wa kujifungua.
Pia wapo watoto ambao huletwa wakiwa katika hali mbaya, wangine wamebakwa na
kulawitiwa. Nilitiwa moyo kuona hata serikali ya wilaya na hata mkoa huleta
watoto katika kituo hicho.
Vipo vyumba
vya watoto wenye hali mbaya, wengine wanaulemavu wa aina mbalimbali, wengine
wameathiki na ukimwi n.k. Shalom Orphanage center ni kama Hospital, Shule, na
mji wa makimbilio. Pia nimeguswa kuona Bibi huyo ameanzisha miradi mbalimbali
ikiwemo ya ng’ombe wa maziwa, kuku wa mayai na mashamba ili watoto wapate lishe
na afya bora. Ukifika shalom lazima ulie kidogo; lakini cha kushangaza watoto
hao,kuanzia wachanga na wale wanaosomeshwa sekondari wote humwita Bibi Warra
Mama!
Mimi kama
mwalimu wa sauti na uimbaji, nikiwanimeambatana na mwenyekiti wa Chama Cha
Wajane Tanzania na baadhi ya watu, pamoja na kila mtu kutoa kile alichokuwanacho,
lakini pia niliamua kuanzisha mpango wa kuibua vipaji vya watoto.
Wito wangu
kwako, ni kukuomba tuungane kwa pamoja safari hii tena, kwa chochote
ulichonacho tukawaone watoto hao mwishoni mwa mwezi huu wa Novemba. Pia
ikumbukwe kuwa karatu nisehemu nzuri ya utalii wa ndani, utajifunza mengi pale MTO
WA MMBU, lakini pia kutembelea mbuga za SERENGETI, NGORONGORO, pamoja na
kutembelea kwenye misitu na mapango ya mawe wanakoishi waadzabe.
Unaweza
ukaleta nguo, chakula, pesa yako na chochote ulichonacho kisha ukakabidhi
katika ofisi za Chama cha Wajane Tanzania zilizopo maeneo ya kinyerezi.
Kwa
mawasiliano zaidi tupigie: 0754 366 530, 0713778778
14 October 2014
KUTUMIA NGUVU ILI KUIMBA VIZURI
12:49
No comments
Hapa ni mwalimu John Shabani sambamba na Masanja mkandamizaji pamoja na Emmanuel Mabisa wakimtumikia Mungu kwa njia ya uimbaji
Huu ni muendelezo wa masomo yanayofundishwa na John shabani, ili kukufanya unayetaka kujifunza kuimba, uwe mwanafunzi mzuri na yule mwimbaji awe bora zaidi.
Tahadhari:
Usilazimishe kutumia nguvu ili uweze kuimba vizuri, kinyume chake jizoeshe
kutumia nguvu kidogo lakini utaalam mwingi (Vocal Technique). Shida ni pale
tunapodhani kwamba nguvu hizi ni kama za wanariadha au wacheza mieleka!
Inawezekana nguvu hizi zisionekane kwa macho ya nyama lakini zinadhihirishwa na
uimbaji wetu. Tunapoimba tunatakiwa kuwa na uhuru (freedom in singing), na sio
kama mtu aliyelazimishwa. Lakini ikumbukwe pia nguvu hizi asili yake inatoka
pia na mfumo wetu wa maisha ya kila siku iki pia ni pamoja na mazoezi ya
viungo, vyakula na vinyaji tunavyotumia, makazi na malazi safi n.k.
Mazoezi mengi
yanayofanyika kwenye vikundi mbalimbali, ni ya kupayuka na kutumia nguvu
nyingi, matokeo yake watu wengi wamekaa kwenye zoezi hilo kwa muda mrefu bila
kuwa na mabadiliko yoyote huku miili yao ikizoofika au kuishia kuwa mtu wa
kupiga kelele na sio kujfunza kuimba vizuri. Haya sio mazoezi ya kumpata
mshindi wa dansi mia mia, ni mazoezi ya kuimba. Imefika mahali sasa masikio
hayawezi kujisikia vile tunavyoimba kwasababu ni kelele na kujichosha.
Ikumbukwe kuwa sauti
hutunzwa kama yai; wengi wetu hufanyishwa mazoezi magumu yasiyolingana na umri
wao na hali yao ya mfumo wa miili yao pamoja na kuzingatia afya zao, matokeo
yake nimeshuhudia watu wakipata matatizo katika koo zao na hata bathi ya miili
yao.
Inashangaza kuona mtu ambaye hajawahi kukimbia maili moja unataka
kumkimbiza maili kumi, matokeo yake ni kudondoka kama sio kupoteza fahamu
kabisa. Yapo mazoezi ya kawaida ya jumla lakini mazoezi mengine ya uimbaji
lazima yazingatie umri wa mtu, hali ya mtu huyo sambamba na afya yake.
Nasikitika kusema kuwa wapo waliofundishwa kwamba akiweza kuimba noti za juu
ndio amekuwa mwimbaji mzuri, matokeo yake mtu anatumia nguvu nyingi, kukaza
misuli ya uso huku usoni akijaribu kuvimba na kutoa macho kama mjusi aliyebanwa
na mlango ili tu awezekufika huko!...
Najua wapo waalimu
wengi katika masomo haya ya uimbaji, na wengine inategemea amejifunza wapi,
lakini bado mwisho wa siku ukweli unabaki kuwa ukweli. Mimi ningeshauri hata kama
wewe ni mwalimu mzuri, mwimbaji mzuri, sote tubaki kuwa wanafunzi.
Kwa ushauri zaidi tupigie
0716560094, au niandikie: touchingvoice@yahoo.com
Pia unaweza ukahudhuria masomo
tunayofundisha sehemu mbalimbali.
12 October 2014
Subscribe to:
Posts (Atom)
HEART OF WORSHIP


























