30 April 2014

J VOCAL TRAINING - DARASA PEKEE LA SAUTI NA UIMBAJI

Mwalimu wa sauti John Shabani kikazi zaidi, ni katika kuhakikisha watu wanfanyika kuwa waimbaji bora na si bora kuimba

 Baada ya mafunzo darasani, wanafunzi hupelekwa studio ili kujipima nguvu

Mwalimu John akisimamia mazoezi ya pumzi



Haya ni masomo machache sana niliyoyachagua kati ya mengi ili kukupa hamasa kujiunga na darasa la uimbaji linaloendelea jirani na Landa mark Hotel Ubungo chini ya mwalimu John Shabani na timu yake

Karibu ujifunze

Mambo ya msingi yanayofunzishwa katika program hii:
·        Tofauti ya mwimbaji na mwanamuziki
·        Vyakula na vinywaji vinavyofaa na visivyofaa kwa mwimbaji
·        Sifa na mbinu za kuwa mwimbaji bora
·        Jinsi ya kuitunza na kuiponya sauti yako
·        Amri 10 za sauti/uimbaji
·        Matumizi ya kipaza sauti (Microphone technique)
·        Utunzi wa nyimbo
·        Sifa 4 za kuwa na Album bora
·        Nguzo 4 za muziki
·        Key 7 za muziki
·        Mazoezi ya viungo yanayofaa kwa mwimbaji na faida zake
·        Ushauri kwa wanaotaka kurekodi nyimbo


Kuimba ni kutamka maneno katika hali ya ki-muziki au pia twaweza kusema ni kutamka maneno moja baada ya jingine kwa sauti yenye lahani (sauti ya ala ya muziki, tuni) au ghani (Singing is the act of producing musical sounds with the voice)

Mwimbaji ni mtu yeyote mwenye uwezo wa kuimba au bila vyombo vya muziki (be sung a cappella) au kwa kutumia vyombo. Mwimbaji huyo kwa lugha ya ki-muziki anaitwa vocalist. Ikumbukwe kuwa pia katika vikundi vya uimbaji wapo wale wanaoongoza wengine katika uimbaji (A lead singer) na wengine kazi yao ni kuitikia (backing singers)
N.B
Mwanadamu yeyote mwenye uwezo wa kuongea, anauwezo wa kuimba pia.

Kama vile tulivyo na ala za aina mbalimbali, mwimbaji naye pia anazo ala mbili muhimu:
         Mdomo wenye uwezo wa kutoa sauti ya uimbaji
         Mwili
Kumbuka moja ya vitu vya msingi katika uimbaji ni nguvu (energy)
Mckinney alisema: “As you sing higher, you must need more energy, as you sing lower, you must useless; as  you sing higher, you must use more space; asa you sing lower, youmust need use less””. Zipo nguvu za kiroho na za kimwili. Ili kuwa na nguvu za kimwili unahitaji maji ya kutosha, chakula kizuri, hewa pamoja na  mazoezi ya viungo au ya pumzi.Mwimbaji pia anahitaji Pumzi ya kutosha (Breathing support), chakula kizuri na maji ya kutosha 


Funguo (Keys) 7 za muziki
C-do, D-re, E-mi, F-fa, G-sol, A-la, B-si
Tunaipata key kwa njia mbili: wewe mwenyewe kujitafutia au kusaidiwa na chombo cha muziki. Wewe mwenyewe ukijipa key, waweza kubadili, lakini ukipewa key na chombo huwezi kwenda kinyume.
Hakuna wimbo unaweza kuimbwa katika key zote saba, bali key moja ye mabadiliko ya key kadhaa. Ninaposhuka key ninaita hiyo ni flat na nikipanda chumba hiyo ni sharp, lakini key E na B hazina sharp. Tofauti ya key moja kwenda key nyingine ni vyumba viwili unapokuwa unatumia vyomvo vya muziki.
Kuimba kwenye tempo ni kuimba kwa kufuata mapigo ya drum au aina yoyote ya ngoma au mshindo
 Ikiwa mwimbaji hajajua kuimbia kwenye funguo (key) na  mapigo au mdundo (beat) bado huyo anatatizo kubwa. Hakuna muziki wa zamani na wa sasa, isipokuwa nyimbo ndio zinaweza kuwa za zamani.
MAADHI YA MUZIKI DUNIANI

Tunaposema maadhi tuna maanisha mtindo f        ulani wa muziki au uimbaji.
Kuna maadhi ya aina nyingi duniani, yapo maadhi ya nchi, maadhi ya kabila maadhi ya dini, maadhi ya koo n.k

Chini ni maadhi kadhaa:
Rumba, Reggae, chakacha, kwela, kwaito, Sukous, sebene, rock, kuna pop n.k

Sauti ni mlio wa chochote kinachoweza kusikika

SIFA ZAKUWA MWIMBAJI BORA

Sauti, kwenda na mapigo na kusimama kwenye ufunguo (Key), mwonekano,  (appearance), Uwezo wa kuitumia sauti na kuitawala (Manage your vocal), Stage presence (Muonekano jukwaani), kujiamini, kujitambua, kujithamini Self Cofidance) n.k.

HATUA 4 ZA KUREKODI AU KUWA NA ALBAM BORA
1.   Mwimbaji kuwa bora
2.   Tungo au ujumbe bora
3.   Muziki bora
4.   Studio bora
NGUZO 4 ZA MUZIKI
1.   Kusikiliza muziki/uimbaji
2.   Kuhifadhi muziki/uimbaji
3.   Kufanyia kazi muziki/uimbaji
4.   Kuzalisha muziki/uimbaji


Mazoezi kwa mwimbaji
Pamoja na faida nyingi za mazoezi lakini pia mazoezi huchangamsha mwili, hulainisha koo, husaidia kuwa na pumzi ya kutosha, hukuhepusha au kupunguza baadhi ya magonjwa kama kisukari, presha n.k, hung’arisha ngozi, na kusaidia mfumo wa mzunguko wa damu, MAZOEZI HUSAIDIA KATIKA MFUMO WA USAGAJI CHAKULA KUWA MZURI , KUKUPA NGUVU NA KUWEZA KUFANYA KAZI KWA NGUVU ZAKO BILA KUJISKIA UMECHOKA NA MWISHO WA SIKU HUPUNGUZA MAFUTA MWILINI,  HUPUNGUZA UZITO, KUNYOOSHA NA KUIMARISHA MISULI YA MWILI, HUSAIDIA MAPIGO MAZURI YA MOYO KWA KUONGEZA KASI YA MAPIGO YAKE WAKATI WA MAZOEZI, UNGUZA MRUNDIKO WA DAMU KWENYE MISHIPA, HII NI MUHIMU KWA SABABU MGANDO WA DAMU HUSABABISHA MAGONJWA YA MOYO PAMOJA NA KUPOTEZA FAHAMU, MAZOEZI HUIMARISHA MIFUPA YA MWILI, HUBORESHA USINGIZI.

Ni vidokezo tu, karibu darasani utajifunza mengi!
0713 778 778

0 comments:

HEART OF WORSHIP

HEART OF WORSHIP