THE OFFICIAL JOHN SHABANI AND GOSPEL IN AFRICA BLOG

Welcome to the official blog of the the gospel singer, songwriter and teacher John Shabani. If you are one of the fans among the millions, feel free to get connected with John Shabani and stay updated on this blog.To learn more about John Shaban and his Ministry, please click the about button above.

GET THE LATEST FROM JOHN SHABAN AND THE GOSPEL NEWS COMMUNITY

You will be able to read and review the latest news on John Shabani's tour and other specials. You will also come across the best articles of news on Gospel from all across Africa and the International Community.Please do feel free to review our categories of news and events.

FEEL FREE TO LEARN MORE ABOUT JOHN SHABANI AND HIS MINISTRY

If you wish to learn more about John Shabani and his ministry, please feel free to connect with John Shabani on the social networks. You can keep up with John Shabani and the Gospel in Africa community on both twitter, facebook, google plus and many other more.

STAY UPDATED WITH INTERNATIONAL AND LOCAL GOSPEL NEWS

Gospel in Africa Blog is a comprehensive gathering place for African Gospel music fans. Offering the latest news and information about Local and International Gospel music and news, Gospel in Africa Blog also shares the spotlight with other genres of Christian music that more than ever, seemingly overlap musical genre lines, such as Bluegrass Gospel, Christian Country and others. Singing News, the leading African Gospel and International music Blog, features African and international Gospel lyrics, radio, news, Christian concerts, songs, artists, and more.

GET IN TOUCH AND STAY CONNECTED WITH JOHN SHABANI

If you are interested in contacting and staying in touch with John Shabani then here are the contacts. E- mail: touchingvoice@yahoo.com or , princejohntz@yahoo.com, Mob: +255 754 818 767 or +255 716 560 094, www.facebook.com/john.shabani.

25 April 2016

SABABU MBALIMBALI ZINAZOPELEKEA MAHUSIANO YA KIMAPENZI KUVUNJIKA

 Picha mbalimbali zinazoonyesha mahusiano yakiwa yamevunjika
 






Nianze kwa kusema, kuna mambo mengi nimeyaandika kwenye kitabu changu kiitwacho “MARUFUKU KUKATA TAMAA”  jipatie nakala yako, kitakusaidia.

Sasa kwa habari ya kuvunika kwa mahusiano kwanza nataka ufahamu MIGOGORO ni jambo la kawaida katika uhusiano wa kimapenzi au ndoa. Na ndiyo maana hata kuvunjika kwa uhusiano wa kimapenzi au ndoa si jambo la kushangaza katika jamii. Mahusiano hayavunjiki hivi hivi, zipo sababu.

Ukizifahamu sababu za kuvunjika kwa mahusiano, kama wewe ni mwathirika wa kuvunjika kwa uhusiano utapona haraka na kujifunza kupenda tena. Kwako wewe ambaye uhusiano wako na mwenzako haujavunjika, au labda hata hujawahi kuingia katika uhusiano, unapozifahamu sababu za kuvunjika kwa uhusiano itakusaidia kufahamu jinsi ya kuenenda unapoingia katika uhusiano wa kimapenzi au hata ndoa, kwa mustakabali mwema
wa uhusiano wako na mwenzako.

Kati ya shughuli nzito ambazo huwakumba watu walio katika mahusiano ya kimapenzi au ndoa ni kuhakikisha kuwa mahusiano yao yanakuwa imara. Ni shughuli yenye changamoto nyingi kwani huhitaji uwiano, maana mwanamume na mwanamke wameumbwa tofauti na kila mmoja ana matakwa na matarajio yake.

Sababu za kuvunjika kwa uhusiano zinaweza kuwapo nyingi na kutofautiana kutoka uhusiano huu na ule, lakini zipo zile ambazo zinaweza kuchukuliwa kuwa kuu. Ukizifahamu utajua jinsi ya kuboresha uhusiano wako wa sasa au baadaye, au kukuweka sawa kisaikolojia kwa ajili ya uhusiano mpya.

Sababu zenyewe ni hizi zifuatazo: -

1. KUKOSEKANA KWA UAMINIFU

Kushindwa kutimiza ahadi, kusema uwongo au kufanya usaliti wa kimapenzi ni mambo
ambayo humwondolea mtu uaminifu kwa mwenzake. Kwa hakika, kukosekana kwa uaminifu ni sababu kuu ya kuyumba na hata kuvunjika kwa mahusiano yaliyo mengi.

Iwapo kuaminiana kwa msingi kabisa katika uhusiano kutavunjwa mara kwa mara, hasira za mpenzi kwa mwenzake zitalimbikizwa na hamu ya wapenzi/wenza kuendelea kuishi pamoja itapungua. Wapenzi walio katika uhusiano wenye mizizi na afya njema wanaweza kukubaliana kumaliza tofauti zao na kusonga mbele. Kama wataheshimu ahadi na viapo vyao vipya mambo yataendelea.

Kumdanganya mpenzi mara kwa mara, kumsaliti mara kwa mara na kuvunja ahadi zako mara kwa mara huufanya uhusiano kudhoofika na hatimaye nguzo yake muhimu – yaani kuaminiana – kuanguka. Hapo ndipo uhusiano hufika kikomo.

2. KUTOKUWEPO KWA UWIANO WA MADARAKA

Katika zama hizi ambapo wanawake wamezifahamu haki zao, kutokuwepo kwa uwiano mzuri katika kutoa maamuzi inaweza kuwa sababu mojawapo ya kuvunjika kwa uhusiano wa kimapenzi au hata ndoa.

Inapotokea kuwa mmoja tu ndiye anayetoa maamuzi kuhusiana na shughuli mbalimbali, uchaguzi wa marafiki, masuala ya kifedha, masuala ya nyumbani, likizo na kadhalika, mwingine anaweza kujiona kama vile hana nafasi katika ushirika huu, hivyo kuamua kujitoa.

Katika zama hizi, wanawake wengi wanafundishwa kuwa na hisia za usawa. Iwapo itatokea mmoja wa wanandoa au wapenzi akajihisi kuwa ametengwa katika maamuzi ya msingi yakiwamo yale yanayohusiana na mustakabali wa maisha yake, ni rahisi sana uhusiano kufika kikomo.

3. KUSHIKILIA IMANI POTOFU

Katika jamii kuna imani potofu mbalimbali kuhusiana na wanawake na wanaume.
Mathalani, kuna imani kuwa wanaume ndio hupenda sana ngono kuliko wanawake au kwamba wanawake ni watu wa kusikiliza na kupelekeshwa tu.

Iwapo mmoja wa wanandoa au wapenzi ataamini katika mojawapo ya imani hizi potofu zenye msingi wa mfumo dume, au imani nyingine zozote, kuna uwezekano mtu huyu akajenga matarajio yasiyokuwa halisi – jambo ambalo hujenga uwezekano mkubwa wa kushindwa kwa uhusiano. Hapa pia kitachotakiwa ni uwiano wa nguvu kutoka pande mbili na kuepuka kuamini katika imani potofu.

4. KUMTENGA MTU NA WATU WAKE

Mojawapo ya sababu kuu za kuachana kwa wapenzi ni mmoja kujihisi ametengwa na
marafiki zake aliotoka nao mbali, ndugu, jamaa na wanafamilia wake, kwa kizingizio
cha mapenzi.

Mara nyingi, wapenzi hujitenga na watu wao wa karibu kutokana na hofu na
kutokujiamini, lakini uhusiano wa aina hii hauwezi kuwa na nguvu na unaweza kujenga mazingira ya kuibuka kwa matatizo mengine ambayo hatimaye yatauua uhusiano.

5. KUTOJITAMBUA KWA MPENZI

Iwapo itatokea kuwa mmoja wa wapenzi/marafiki au wote wawili akawa hajitambui na kufuata matakwa yake, mahitaji yake, matamanio yake, mipango yake ya baadaye, malengo yake, msimamo wake, hulka yake na vipaumbele vyake, haitakuwa rahisi kwa watu hawa wawili kuwa na uhusiano wenye afya.

Kujitambua huwasaidia wapenzi kuwa huru kila mmoja kwa mwenzake, akimweleza anataka nini, jambo ambalo husaidia kuimarisha uhusiano. Lakini inapotokea kuwa mmoja wa wapenzi hajitambui, au wote wawili hawajitambui, ni rahisi sana uhusiano kuvunjika, hasa kama wahusika waliingia katika uhusiano huo wakiwa na umri mdogo.

6. KUTOJITHAMINI NA KUTOJIAMINI

Inapotokea mmoja wa wapenzi akajihisi kuwa hastahili kupendwa, hiyo inatosha kuwa sababu ya mazingira ya kuvunjika kwa uhusiano. Hali hii hutokana na kutojithamini na kutojiamini kwa mtu – mambo ambayo yanaweza kusababishwa na sababu mbalimbali yakiwamo malezi.

Kutokujiamini au kuwa na hofu ya kuachwa kunaweza kumfanya mtu ambane sana mwenzake na kumnyima uhuru – jambo ambalo halifai kwa afya na ustawi wa uhusiano. Kujiamini na kujithamini kwa mwenza ni njia mojawapo ya kuepuka kuvunjika kwa uhusiano.

7. WIVU ULIOKITHIRI

Wivu ni mojawapo ya sababu kuu za kuvunjika kwa uhusiano wa kimapenzi au hata ndoa. Wivu wa kupindukia unaweza kusababisha ugomvi ambao nao ni sababu kubwa ya kuachana kwa wapenzi.

Wivu husababishwa zaidi na kutokujiamini kwa mtu. Kwa hiyo, ili kuepuka wivu na
kuunusuru uhusiano wa kimapenzi, lazima mtu kwanza ajithamini na kujiamini kuwa
anastahili kupendwa na mpenzi wake kama alivyo.

8. MAWASILIANO HAFIFU

Mawasiliano ni kitu muhimu sana katika mapenzi. Iwapo wapenzi watashindwa kuelezana hisia zao, mawazo yao, mitazamo yao, imani zao, matatizo yao au hata furaha zao, uhusiano utakuwa unaelekea pabaya.

Inapotokea hiyo ikawa sababu ya kuachana kwa wapenzi, basi mtu anapojifunza tena
kupenda atapaswa kujifunza pia jinsi ya kuwasiliana vema na mwenzake, kwani kwa
hakika mawasiliano mabaya ni sababu kubwa ya kuachana kwa wapenzi.

9. MMOJA KUMDHIBITI MWENZAKE

Inapotokea kuwa mmoja wa wapenzi anataka kumdhibiti mwenzake na kumwendesha mithili ya mtu anayemwendesha farasi, uhusiano unaohusika utakosa mapenzi – na hiyo itakuwa sababu kubwa ya kuachana kwa wapenzi hawa baadaye.

Sababu hii inaweza kuchukuliwa katika namna tofauti. Mtu anaweza kumbana mwenzake kwa kumfuatilia muda wote, kumtishia – mathalani anapochelewa nyumbani au kwenye miadi – na kutompa ruhusa na uhuru wa kupanga ratiba zake au kutoka na watu wa karibu naye. Hii si tabia ya kimapenzi na matokeo yake ni kushindwa kwa uhusiano.

10. UNYANYASAJI

Hii ndiyo sababu ambayo pengine iko wazi zaidi. Kuna aina mbalimbali za unyanyasaji
ambao hujitokeza baina ya wapenzi na si lazima kwamba mwanamume ndiye anayemnyanyasa mwanamke kama ilivyozoeleka. Hata wanawake huwanyanyasa wanaume.

Unaweza kudhani ukinyanyaswa tu na mpenzi au mwenza utamwacha, lakini ukweli ni kwamba wengi huvumilia, pengine kutokana na kuiogopa jamii inayowazunguka. Lakini ukweli ni kwamba unyanyasaji huondoa kabisa maana ya mapenzi na kusababisha wapenzi
wengi kukosa sababu ya kuendelea kuwa pamoja.

KUWA MAKINI

Migogoro ni kitu cha kawaida katika uhusiano wa kimapenzi – na kwa hakika haiepukwi, isipokuwa wenza hujifunza jinsi ya kuimaliza na kuondoka wakiwa salama. Hata hivyo, kuna nyakati ambapo uhusiano hufifia na wakati mwingine hufikia kikomo msipokuwa makini. Yapo mambo yaliofanyika wakati watu wanamoto wa kuchumbiana, kadiri wanapoendelea katika urafiki, uchumba na baadaye ndoa mengine yanatoweka na mengine yanajitokeza. Una heri wewe ambaye umezifahamu sababu kuu za kuvunjika kwa uhusiano maana zitakusaidia kufahamu jinsi ya kujipanga na kutengeneza uhusiano wenye afya na mustakabali mwema.

Kwa mengi zaidi nipigie, nitumie ujumbe au ni whatsapp 0716560094

 


HEART OF WORSHIP

HEART OF WORSHIP