THE OFFICIAL JOHN SHABANI AND GOSPEL IN AFRICA BLOG

Welcome to the official blog of the the gospel singer, songwriter and teacher John Shabani. If you are one of the fans among the millions, feel free to get connected with John Shabani and stay updated on this blog.To learn more about John Shaban and his Ministry, please click the about button above.

GET THE LATEST FROM JOHN SHABAN AND THE GOSPEL NEWS COMMUNITY

You will be able to read and review the latest news on John Shabani's tour and other specials. You will also come across the best articles of news on Gospel from all across Africa and the International Community.Please do feel free to review our categories of news and events.

FEEL FREE TO LEARN MORE ABOUT JOHN SHABANI AND HIS MINISTRY

If you wish to learn more about John Shabani and his ministry, please feel free to connect with John Shabani on the social networks. You can keep up with John Shabani and the Gospel in Africa community on both twitter, facebook, google plus and many other more.

STAY UPDATED WITH INTERNATIONAL AND LOCAL GOSPEL NEWS

Gospel in Africa Blog is a comprehensive gathering place for African Gospel music fans. Offering the latest news and information about Local and International Gospel music and news, Gospel in Africa Blog also shares the spotlight with other genres of Christian music that more than ever, seemingly overlap musical genre lines, such as Bluegrass Gospel, Christian Country and others. Singing News, the leading African Gospel and International music Blog, features African and international Gospel lyrics, radio, news, Christian concerts, songs, artists, and more.

GET IN TOUCH AND STAY CONNECTED WITH JOHN SHABANI

If you are interested in contacting and staying in touch with John Shabani then here are the contacts. E- mail: touchingvoice@yahoo.com or , princejohntz@yahoo.com, Mob: +255 754 818 767 or +255 716 560 094, www.facebook.com/john.shabani.

28 December 2011

UBARIKIWE NA BWANA

21 December 2011

BELLA KOMBO AMRUDIA BWANA


Christabella Kombo kwa jina maaarufu Bella Kombo, hivi karibuni ameamua kuachana na muziki wa dunia na kuanza kumwimbia Bwana. Mwanadada huyo aliyeonekana kuvutia sana kwenye mashindano ya Bongo Star Seach BSS ya 2010 na 2011, hivi sasa amerekodi album yake ya nyimbo za injili. Kabla hajajiunga na Bss, Bella alikua mwimbaji mzuri kanisani na pia sauti ya Bella imesikika sana ktika baadhi ya nyimbo mbalimbali za mwalimu John Shabani.

Akiongea na mwandishi wa blog hii, bella amekiri kumrudia Bwana maana yeye siku zote alikua ni mwimbaji kanisani. Kilichotokea ni kwamba, baada ya watu na wadau mbalimbali kugundua kipaji chake, walimshauri na kumshawishi ajiunge na Bss kwamba huko kipaji chake kitajulikana zaidi pamoja na kujitangaza kwasababu kazi ya Bss ni kuinua vipaji haijalishi unaimba maadhi gani ya muziki. Baada ya kipaji chake kujulikana zaidi, alishawishiwa kujiunga na kundi la Machozi Band, hata hivyo moyo wake umekuwa ni wa kumwimbia mwenyezi Mungu. Baada ya kushauriwa na watu pamoja na watumishi mbalimbali hasa zaidi mwalimu wake bwana John Shabani ambaye hapo awali amekuwa akiimba pamoja na bella, ndipo alipoamua kurudi kundini na kuanza tena kumwimbia Bwana.

Hivi sasa Bella anategemea kujiunga na kundi la Glorious Celebration la jijini Dar es salaam.

19 December 2011

JOHN SHABANI, FARAJA NTABOBA, UPENDO KILAHIRO NA CHIDUMULE NDANI YA VIDEO MOJA

                                 John Shabani na Upendo kilahiro baada ya kuimba wimbo maalum wa miaka 50 ya huru wa Tanzania kwenye uwnja wa uhuru.





                                    John Na Faraja Ntaboba wakirekodi mkanda wa video






Wapenzi wa nyimbo za injili wakae mkao wa kula, Album mpya ya John shabani alioshirikisha waimbaji nyota wa nyimbo za injili wa Tanzania, DRC kongo na Uganda sasa kukamilika mwanzoni mwa January katika mfumo wa audio na video. Hii ni albam ya kipekee na ni kwamara ya kwanza kuwepo na albam ya mwimbaji ilioshirikisha waimbaji mbalimbali nyota. Hii ni ktokana na moyo wakipekee alionao Mwalimu John shabani, kwani amekua akijitolea kuinua vipaji mbalimbali vya waimbaji bila kubagua. Baadhi ya waimbaji katika albam hiyo ni: Faraja Ntaboba (Mwimbaji maarufu anaye tikisa Afrika kutoka kule kongo Drc, Cosmas Chidumule, Upendo kilahiro, Askofu John komanya(Aliyetamba na kibao cha zawadi gani nitamtolea Bwana), Jane miso (Mama wa Omayo), Christina Matai(Mwang'onda), Tina Marego, X-tano Family group (Kampala Uganda) na wengine kabao.

Albam hiyo inasimamiwa na kusambazwa na kampuni ya Msama Promotions.

15 December 2011

WATANZANIA (MIAKA 50 YA UHURU)

• COSMAS CHIDUMULE NA JOHN SHABANI WAKONGA MIOYO YA MAELFU YA WATU

Mkongwe wa muziki wa injili Afrika Mzee Cosmas Chidumule pamoja na mwalimu maarufu wa Muziki wa injili afrika mashariki bwana John Shabani,Wamegusa mioyo ya maelfu ya waumini walioshiriki ibada katika kanisa la mlima wa moto (Mountain of fire) la mikocheni b assemblies of God linaongozwa na Dr, Rv. Getrude Rwakatare. Kibao cha Kwa Yesu kuna raha chake john Shabani alichomshirikisha Chidumule ndicho kilicho tifua maelfu ya waumini hao. Wimbo huo umo ndani ya album mpya yakwake John shabani alioshirikisha waimbaji nyota wa nyimbo za injili Tanzania, Congo na Uganada. Album hiyo inatarajia kukamilika mwishoni mwa mwaka huu kwa mfumo Audio na video na inasimamiwa na kusambazwa na Kampuni ya Msama Promotions




13 December 2011

WIMBO ULIOIMBWA NA TANZANIA GOSPEL ALL STARS WAPATA HESHIMA YA KUWA WIMBO MAALUM KATKA MAADHIMISHO YA MIAKA 50 YA UHURU WA TANZANIA

                                   Umati wa maelfu ya watu

                                        Upendo kilahiro akiwa na mwalimu John Shabani
                                    G stars wakiimba mbele ya marais na waheshimiwa mbalimbali
                                       Mwalimu maarufu wa nyimbo za injili Afrika mashariki
                                      (John shabani), akiimba kwa hisia kali mbele ya rais



                          Mzee makasy (Mwimbaji mkongwe), Akiimba mbele ya rais



                             Mheshimiwa martha mlata akiimba kwa hisia

                                Mtoto wa miaka 6 Gloria kilahiro akiimba kwa hisia kali mbele ya waheshimiwa



                              



Wimbo wa kuadhimisha miaka 50 ya uhuru wa Tanzania ulioimbwa na Tanzania Gospel All stars (Waimbaji nyota wa muziki wa injili Tanzania), umepata hadhi na heshima ya kuwa wimbo maalumu katika maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru wa Tanzania bara.

Chini ya mwalimu John shabani na usimamizi wa chama cha muziki wa injili Tanzania(Chamuita), Waimbaji hao walipewa nafasi maalum ya kuimba wimbo huo mbele ya Rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania Dokta Jakaya Mrisho Kikwete na mbele ya marais wa nchi mbalimbali, mawaziri, wabunge, mabalozi,  pomoja na maelfu ya watu waliohudhuria katika maadhimisho hayo. Viongozi na watu mbalimbali wamewapongeza waimbaji hao wa injili kwa umoja na mshikamano wao, pia wameupongeza wimbo huo, hivyo kuwaomba kuusambaza wimbo huo kwa watanzania ili kila mtu abarikiwe na wimbo huo

Hii ni mara ya kwanza kwa waimbaji wa injili kuungana pamoja na kurekodi wimbo wa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa ajili ya uhuru wa Tanzania.
Video ya wimbo huo inategemea kusambazwa kwa watanzania kwa gharama ndogo.

Waimbaji walioshiriki kurekodi wimbo huo ni:

1. Gloria kilahiro                                            18. Mzee Makassy
2. Amon Kilahiro                                            19. Mzungu Four
3. Masanja Mkandamizaji                                20  Jane Misso
4. Upendo kilahiro                                            21 Addo November
5. Stella Joel                                                  22. Mheshimiwa Martha Mlata
6. Nely Nyamanga                                         23. Ambwene mwasongwe
7. Joyce Ombeni                                                                                                                    
8.  Bony Mwaitege                                          24. Douglas Pius
9. John Shabani                                              25. Mchumu Maximillian
10. Rose Manoza                                              26. Charles Thobias Malya
11. Yona Abiud                                                  27. Joshua makondeko
12. Miriam Lukindo Mauki                                  28. Daniel Safari
13. Robert Bukelebe                                          29. Naomy Mbwambo
14. Nicholaus Misuzi                                          30. Joseph kasigala
15. Christina Matai                                             31. Debora Said
 16. Tina Marego                                               32. Stara Thomas  
17. Martha Mwaipaja                                        33. Victor Ahron
Na wengine wengi.

Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania

8 December 2011

Tanzania gospel all stars kuimba kwenye maadimisho ya miaka 50 ya uhuru

Hatimaye waimbaji wa injili (Tanzania All Gospel Stars) walioshiriki kurekodi wimbo wa miaka 50 ya uhuru wa Tanzania chini ya uongozi wa Camuita(Chama cha muziki wa injili Tanzania), wameingizwa katika ratiba ya uimbaji katika sherehe za maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru. Maadhimisho hayo yatafanyika kesho katika viwanja vya uhuru/kiwanja cha taifa. Waimbaji hoa wameombwa kuwahi mapema yaani saa moja kamili asubui, ili kupewa ratiba kamili pamoja na taratibu nyingine. Pia kila mshiriki avae sare ya maadhimisho. Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika.

29 November 2011

Martha Mwaipaja avishwa pete ya uchumba


Mwimbaji wa muziki wa Injili nchini, Martha Esau Mwaipaja (pichani)  amechumbiwa na Mchungaji, John Said anayehudumia Kanisa la Udhihirisho wa Injili lililopo Ukonga jijini Dar es Salaam, Risasi Jumamosi linakupa habari kamili.

Habari zisizo na chenga zilizotua kwenye meza ya ya blog hii zilisema, Martha alivishwa pete ya uchumba na mchungaji huyo  katika Kanisa la Victoria lililopo Ubungo External jijini Dar na baada ya zoezi hilo kulikuwa na sherehe ndogo kanisani hapo kwa ajili ya kumpongeza kwa kufikia hatua hiyo,”
Mwana dada huyo anayetamba na vibao kama vile Usikate tama, wewe ni baba n.k amekiri kuchumbiwa na mchungaji huyo na kuongeza shughuli ya kesho ilinogeshwa na waimbaji wenzake kama vile Bahati Bukuku, Sarah Mvungi, Ambwene Mwasongwe na Christina Matai.
Wengine ni David Robert, Debora John, Josephine Mwasulama, Ado November, Jennifer Mgendi, Lianga George, Stella Swai na wengineo.

11 November 2011

ZIARA YA KUENEZA CHAMA CHA MUZIKI WA INJILI MIKOANI

                           bwana John Shabani akihojiwa na bi Revina Steven mtangazaji
                        wa Top radio kuhusu chama cha muziki wa injili Tanzania


                     Mkurugenzi wa Top radio bwana Steven Lukindo akiwa katika picha
                     na makatibu wenezi wa chamuita.

                                         bwana Magida Timotheo amabaye ni mjumbe wa chamuita
                            anayewakilisha watu wenye ulemavu, akiwa ameshikilia katiba ya chama
                            kabla ya kukikabidhi kwenye uongozi wa morogoro
                                      

                           John Shabani akikabidhi fomu za kujiunga na chama

                    Wawakilishi wa kwaya, bendi na waimbaji binafsi wakionyesha nyuso za
                   furaha baada ya kuletewa chama cha muziki wa injili morogoro.



                                  Viongozi wa chama wakiwa katika picha ya pamoja na mkurugenzi wa
                              Vatican Lodge bwana Thomas B. Butabile. Hapo ndipo walipofikia viongozi hao.
                                                Maswali mbalimbali yakiulizwa

Chama cha Muziki wa Injili kupitia kamati ya uenezi chini ya makatibu wenezi bwana John Shabani na bi stella Joel, wameanza ziara ya kukieneza chama hicho mikoani, wakianzia na mkoa wa morogoro. Ziara hiyo imetokana na maagizo ya shirikisho la muziki Tanzania (Tanzania music federation) na braza la sanaa la taifa (BASATA), kwamba chama hai ni kile kilichoenea nchi nzima. Wakwa mkoani morogoro, viongozi hao wakiwa wameongozana na mwimbaji bwana Magida Timotheo ambaye ni mjumbe wa chama hicho anayewakilisha watu wenye ulemavu, wamepewa ushirikiano mkubwa na Top Radio chini ya uongozi wa bwana Steven Lukindo. Pia Dada Revina Steven na Dada Bupe kama watangazaji wa redio hiyo, wamefanya kazi kubwa ya kuhamasisha wakaaji wa morogoro na vitongoji vyake, waweze kujiunga na Chama hicho. mamia ya wakaaji wa morogoro wameonyesha kuitikia mwito wa kujiunga na chama hicho na kuomba ziara hiyo isiishie morogoro peke yake bali katika nchi nzima. Viongozi hao wa chama wamekabidhi katiba ya chama na fomu za kujiunga na baada ya muda si mrefu uongozi wa mkoa wa morogoro utaundwa chini ya usimamizi wa makao makuu

31 October 2011

NIWEZESHE (Moja ya nyimba za John shabani zinazobari watu) Watch it!

MUME WA MAREHEMU ANJELA CHIBALONZA AJIPATIA UBAVU MPYA

Hatimaye aliyekuwa mume wa marehemu Angela Chibalonza, ajipatia ubavu mwingine. Mtumishi huyo wa Mungu ameoa hivi karibuni huko DRC kongo. Picha hizi ni baada ya wiki chache za ndoa alipohudumu ni mke wake mpya katika kanisa la Mikocheni B assemblies of God, linaloongozwa Na Mchungaji Getrude Rwakatare.
Kuhusu jina la mke wake na habari zote za harusi hiyo tutakujulisha hivi karibuni.
                    Mchungaji Muliri akiimba mke mpya hivi karibuni katika kanisa la mikocheni B

                          Mke wa Elisha muliri akiimba kwa hisia kali



24 October 2011

TANZANIA GOSPEL STARS WAKAMILISHA VIDEO YA WIMBO WA MIAKA 50 YA UHURU WA TANZANIA

Hatimaye waimbaji wa nyimbo za injili Tanzania  wakiongozwa na mwalimu wa muziki wa injili afrika mashariki bwana John Shabani, chini ya usimamizi wa chama cha muziki wa injili Tanzania (Chamuita) wamekamilisha video ya wimbo ya miaka 50 ya uhuru wa Tanzania. Pamoja na waimbaji mbalimbali kushiriki katika wimbo huo pia yumo mheshimiwa Martha Mlata ambaye amechangia sana katika kufanikisha kurekodi wimbo huo. Baadhi yam abo aliyo yafanya ni pamoja na kufanikisha kupata sare na bendera kutoka serekalini pamoja na kutoa feha za kufanikisha kurekodi video. Pia studio ya Pro arts studio ya jijini Dar es salaam ilijitolea kurekodi sauti. Wazo la kuwakusanya waimbaji wa injili na kurekodi wimbo wa miaka 50 ya uhuru, lilianzishwa na bwana Tc Timothy  Chelula na kumshirikisha mwalimu John Shabani, ndipo walipo kihusisha chama cha muziki wa injili na vyombo mbalimbali vya habari. Muda si mrefu wimbo huo utasambazwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari nchini.
Baadhi ya waimbaji walioshiriki kurekodi wimbo huo ni:
1. Gloria kilahiro                                            18. Mzee Makassy
2. Amon Kilahiro                                            19. Mzungu Four
3. Masanja Mkandamizaji                                20  Jane Misso
4. Upendo kilahiro                                            21 Addo November
5. Stella Joel                                                  22. Martha Mlata
6. Nely Nyamanga                                         23. Ambwene mwasongwe
7. Joyce Ombeni                                                                                                                       
8.  Bony Mwaitege                                          24. Douglas Pius
9. John Shabani                                              25. Mchumu Maximillian
10. Rose Manoza                                              26. Charles Thobias Malya
11. Yona Abiud                                                  27. Joshua makondeko
12. Miriam Lukindo Mauki                                  28. Daniel Safari
13. Robert Bukelebe                                          29. Naomy Mbwambo
14. Nicholaus Misuzi                                          30. Joseph kasigala
15. Christina Matai                                             31. Debora Said
 16. Tina Marego                                               32. Stara Thomas  
17. Martha Mwaipaja                                        33. Victor Ahron
Na wengine wengi.
                                Mheshimiwa Martha, Mr Masanja na Malimu John wakitabasamu
                  Kampuni ya Pro arts wakiwa kazini
                                  Masanja mkandamizaji akifanya vitu vyake


                            Baadhi ya magari mbalimbali ya waimbaji nnje ya jengo la studio

                     Mwimbaji mkongwe mzee makasi katika pozi
                      Mwalimu John Shabani akiwaongoza waimbaji wa Injili


Pamoja na hayo, viongozi wa chama cha muziki wa injili Tanzania tunatoa wito wa kujiunga na chama hicho, kwani kuna faida nyingi za kujiunga na chama. Fomu sasa zinapatyikana. kwa mawasiliano zaidi piga simu namba 0754818767, 0716560094.

HEART OF WORSHIP

HEART OF WORSHIP