22 March 2017

SOMO: AINA YA NYIMBO SIFA NA MAANA YAKE

Watu wengi mmekua mkiniuliza maswali haya kuhusu aina ya nyimbo, maana ya nyimbo, mahudhui ya nyimbo. Samahani, kuna mambo yamenishika kidogo. Lakini leo acha niwajibu kwa ufupi.



Kwa masomo zaidi tembelea kurasa zangu za facebook:
-          JOHN SHABANI & SINGING MINISTRY
-          Dar es salaam Singing Lessons & Music Academy

Nyimbo ni aina ya sanaa katika fasihi ambayo hutumia lugha teule, sauti na kiimbo maalum.
Aghalabu nyimbo hutumia ala za mziki kama vile ngoma. Nyimbo zinaweza kuimbwa na mtu mmoja au zaidi. Wimbo hugawanywa katika beti na mishororo. Nyimbo nyingi huwa na kiitikio au mstari ambao hurudiwa rudiwa.
Sifa za Nyimbo
  1. Hutumia kiimbo au sauti maalum
  2. Huweza kuendamana na ala za muziki
  3. Huimbwa na mtu mmoja au watu wengi; wakati mwingine nyimbo huimbwa kwa kupokezanwa.
  4. Hutumia lugha ya mkato
  5. Hurudiarudia (kukariri) maneno ili kusisitiza ujumbe katika wimbo
Umuhimu wa Nyimbo katika Fasihi Simulizi
  1. Kuburudisha
  2. Kuelimisha, kufunza, kuonya, kuelekeza
  3. Kuliwaza
  4. Kusifia kitu au mtu katika jamii
  5. Kuunganisha jamii
  6. Kudumisha/kuhifadhi tamaduni za jamii
  7. Kukuza talanta na sanaa katika jamii
  8. Hutumika katika mbinu nyingine za fasihi kama vile hadithi
Vipera/Aina za Nyimbo
Kulingana na Muundo:
Kulingana na Ujumbe/Maudhui:
Nyimbo za Ndoa
Nyimbo za harusi huimbiwa bwana na bibi harusi kuwapongeza na kuwapa heko kwa kufunga ndoa yao. Aidha nyimbo hizi huwapa wawili hao mawaidha ya kutunza familia na watoto wao ili waishi pamoja.
Nyimbo za Jandoni/Tohara
huimbwa na vijana wanapopashwa tohara. Nyimbo hizi huonyesha ushujaa, na kuashiria kutoka kwamba anayetahiriwa amekuwa mtu mzima sasa.
Hodiya/Wawe
Hizi ni nyimbo ambazo huimbwa na watu wanapofanya kazi ili kuwatia bidii wafanye kazi bila kuhisi machofu.
Kimai
Nyimbo za Mabaharia - Hizi ni nyimbo za wanabahari wanaposafiri baharini.
Nyimbo za Mazishi/Huzuni/Simanzi
Hizi ni nyimbo za kuliwaza na kuwapa pole walioachwa na marehemu. Nyimbo hizi huwapa matumaini waombolezaji.
Nyimbo za Kidini
Hizi ni nyimbo ambazo huimbwa kumsifia Mungu, kuomba au kutoa mafunzo ya kidini.
Nyimbo za Kisiasa
Hizi ni nyimbo za kuwasifia viongozi wa kisiasa
Nyimbo za Kizalendo
Nyimbo za huonyesha uzalendo kwa kusifia taifa/nchi
Nyimbo za Mapenzi
Katika nyimbo za mapenzi, mwimbaji huimba kwa kumsifia mpenzi wake hasa kwa urembo na tabia zake
JOHN SHABANI & SINGING MINISTRY
Dar es salaam Singing Lessons & Music Academy


0 comments:

HEART OF WORSHIP

HEART OF WORSHIP