14 October 2014

KUTUMIA NGUVU ILI KUIMBA VIZURI



Hapa ni mwalimu John Shabani sambamba na Masanja mkandamizaji pamoja na Emmanuel Mabisa wakimtumikia Mungu kwa njia ya uimbaji

Huu ni muendelezo wa masomo yanayofundishwa na John shabani, ili kukufanya unayetaka kujifunza kuimba, uwe mwanafunzi mzuri na yule mwimbaji awe bora zaidi.

Tahadhari: Usilazimishe kutumia nguvu ili uweze kuimba vizuri, kinyume chake jizoeshe kutumia nguvu kidogo lakini utaalam mwingi (Vocal Technique). Shida ni pale tunapodhani kwamba nguvu hizi ni kama za wanariadha au wacheza mieleka! Inawezekana nguvu hizi zisionekane kwa macho ya nyama lakini zinadhihirishwa na uimbaji wetu. Tunapoimba tunatakiwa kuwa na uhuru (freedom in singing), na sio kama mtu aliyelazimishwa. Lakini ikumbukwe pia nguvu hizi asili yake inatoka pia na mfumo wetu wa maisha ya kila siku iki pia ni pamoja na mazoezi ya viungo, vyakula na vinyaji tunavyotumia, makazi na malazi safi n.k.
Mazoezi mengi yanayofanyika kwenye vikundi mbalimbali, ni ya kupayuka na kutumia nguvu nyingi, matokeo yake watu wengi wamekaa kwenye zoezi hilo kwa muda mrefu bila kuwa na mabadiliko yoyote huku miili yao ikizoofika au kuishia kuwa mtu wa kupiga kelele na sio kujfunza kuimba vizuri. Haya sio mazoezi ya kumpata mshindi wa dansi mia mia, ni mazoezi ya kuimba. Imefika mahali sasa masikio hayawezi kujisikia vile tunavyoimba kwasababu ni kelele na kujichosha.
Ikumbukwe kuwa sauti hutunzwa kama yai; wengi wetu hufanyishwa mazoezi magumu yasiyolingana na umri wao na hali yao ya mfumo wa miili yao pamoja na kuzingatia afya zao, matokeo yake nimeshuhudia watu wakipata matatizo katika koo zao na hata bathi ya miili yao. 

Inashangaza kuona mtu ambaye hajawahi kukimbia maili moja unataka kumkimbiza maili kumi, matokeo yake ni kudondoka kama sio kupoteza fahamu kabisa. Yapo mazoezi ya kawaida ya jumla lakini mazoezi mengine ya uimbaji lazima yazingatie umri wa mtu, hali ya mtu huyo sambamba na afya yake. Nasikitika kusema kuwa wapo waliofundishwa kwamba akiweza kuimba noti za juu ndio amekuwa mwimbaji mzuri, matokeo yake mtu anatumia nguvu nyingi, kukaza misuli ya uso huku usoni akijaribu kuvimba na kutoa macho kama mjusi aliyebanwa na mlango ili tu awezekufika huko!...

Najua wapo waalimu wengi katika masomo haya ya uimbaji, na wengine inategemea amejifunza wapi, lakini bado mwisho wa siku ukweli unabaki kuwa ukweli. Mimi ningeshauri hata kama wewe ni mwalimu mzuri, mwimbaji mzuri, sote tubaki kuwa wanafunzi.

Kwa ushauri zaidi tupigie
0716560094, au  niandikie: touchingvoice@yahoo.com
Pia unaweza ukahudhuria masomo tunayofundisha sehemu mbalimbali.

0 comments:

HEART OF WORSHIP

HEART OF WORSHIP