3 February 2015

HATIMAYE CHINI YA USIMAMIZI WA MWL. JOHN SHABANI WATOTO WA SHALOM ORPHANAGE WAREKODI ALBAM YAO YA KWANZA

Mwl. John Shabani akitoa darasa 
kwa watoto wa Shalom Orphanage




Nilitembelea kituo cha Shalom Orphanage Centre mwaka 2014, hakika nilijifunza mambo mengi, huku nikijaribu kuona tofauti iliopo kati ya vituo mbalimbali vya watoto yatima nilivyowahi kuvitembelea Tanzania na nje ya mipaka yetu.

Mlezi wa kituo hicho Mama Warra Nnko, kwanza ni Mjane, pili baada ya kuguswa na haili ya maisha ya watoto yatima, aliamua kusahau hali yake ya ujane na kujiona kuwa anayo nafasi kubwa ya kufanya lolote awezalo ili kuyakomboa maisha ya mtoto yatima Tanzania. Ndipo Mama huyo alipoamua kutoka katika Jiji la Arusha, huku akiacha makazi yake mazuri na kujielekeza huko karatu, ni takriba kilomita 160 kutoka Jiji la Arusha. Tangu mwaka 2004 Mama huyo akilea watoto yatima katikamakazi aliyofanikiwa kuyapata huko karatu. Ukifika Shalom Orphanage Centre hakika huwezi kuyazuia machozi yako, hasa bale unapoona zaidi ya watoto 60, wengine wachanga, wengine wenye ulemavu, wengine walioathirika na ukimwi, wote hao humwita Mama warra jina moja tu (Mama)
Ikumbukwe, jirani na wilaya ya karatu ndiko kunakoongoza kwa vivutio vya utalii Tanzanzania, hivyo, kwasababu ya habari zilizoeneo kote duniani kuhusu kituo hicho, watalii na wasamaria wengi wanaotembelea Ngorongoro, Serengeti, n.k, mara nyingi pia hukitembelea kituo hicho. 

Niliposikia habari za kituo hicho, nikiwa mwana harakati wa haki za Binadamu, nilifunga safari na kutembelea shalom Orphanage, nikajisikia kunzisha program ya kuibua vipaji hasa vya uimbaji. Kwa kuanzia, tayari mapema mwaka huu wa 2015, tumerekodi Albam ya kwanza na maandalizi ya mkanda wa video yanaendelea. Naamini kwa kupitia ujumbe uliomo ndani ya nyimbo hizi utagusa mioyo ya watu wengi ndani na nje ya nchi. Lakini pia mkanda wa video utakiunganisha kituo na dunia, kwani nyimbo hizo zitatafsiriwa kwa lugha ya kingereza. Pia nyimbo hizi zitawaingizia kipato.
Baadhi ya nyimbo zilizomo katika Albam hiyo ni: Mtoto wa mwenzio ni wako, Sitaitwa Yatima tena, Nani kama Mama, Baba wa Yatima na Tanzania.

Endelea kuombea kituo hicho, na pia unaweza ukatoa
mchango wako wa hali na mali ili kuwabariki watoto hao.




0 comments:

HEART OF WORSHIP

HEART OF WORSHIP