20 June 2015

NAIBU WAZIRI WA ARDHI NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI, ANGELA KAIRUKI KUWA MGENI RASMI KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA WAJANE DUNIANI





 Mwenyekiti wa Chama cha Wajane Tanzania, Rose Sarwatt na katibu wa chama hicho bwana John Shabani, wakizungumza na waandishi wa habari juu ya madhimisho ya siku ya wajane duniani. kulia ni mjumbe wa chama hicho, bi Mwajua Mwinyimkuu
 Mheshimiwa Ajnjela Kairuki, mgeni rasmi katika maadhimisho ya kwanza Tanzania, ya siku ya wajane Duniani.


NAIBU Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angela Kairuki anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya wajane Duniani.
Tunategemea pia kuwa na wadau mbali mbali, kama vile viongozi wa serikali, viongozi wa kidini, wawakilishi wa taasisi mbalimbali za serikali na binafsi, waandishi wa habari pamoja na wasanii mbalimbali, wamesema.



Maadhimisho hayo yanatarajiwa kufanyika Juni 23 mwaka huu, yaani siku ya jumanne, ambapo kimkoa yatafanyika  katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam.
Wakizungumza na waandishi leo Jijini Dar, Mwenyekiti wa Chama cha Wajane Tanzania (TAWIA), Rose William Sarwatt na katibu mkuu wa chama hicho, bwana John Shabani, wamesema, siku hiyo itawakutanisha wajane wote nchini. Katika maadhimisho hayo pia wataweza kujadili changamoto mbalimbali zinazowakabili pamoja na utatuzi wake.

Maadimisho hayo ambayo yanafanyika Dunia nzima kwa hapa nchini yatabeba kauli mbiu isemayo, “Andika wosia kuepusha migogoro isiyokuwa na lazma”. Yataanzia stendi ya stesheni hadi sehemu husika. “Kauli mbiu hiyo imekubalika na takrbani ya wajane wote nchini, kutokana na changamoto zetu kufanana, ikiwemo ya kushuka kwa uchumi ndani ya familia pindi mume anapofariki,” amesema Sarwatt.  
Aidha amesema, changamoto kubwa wanayoipigia kelele wajane wengi nchini ni uchumi kuporomoka pindi wakiondokewa na wenza wao, hivyo tatizo hilo pia huongeza   idadi ya watoto yatima mitaani.

Mbali na kupata changamoto hizo Sarwatt amesema, uwepo wa TAWIA umekuwa msaada mkubwa na kimbilio la wajane wengi kwani kimekuwa msari wa mbele kuwasaidia. Licha ya wajane wengi kuonekana kukata tamaa ya maisha, TAWIA ilianzisha miradi mbalimbali ya kuweza kuinuana kimaisha ikiwemo ya kufanya biashara ndogondogo. Na kwamba biashara hizo na michango mbalimbali imewasaidia kuwapeleka watoto shule pamoja na kujikimu katika maisha yao.
“Tuchukue fursa hii kuwakumbusha wadau mbalimbali ambao wanaweza kutusaidia, ili tuweze kuwafikia wajane wengine waliopo vijijini ambao hatuwezi kuwafikia. Pia tunaomba serikali itusaidie kupata takwimu ya wajane  wote nchini, ili iwe rahisi kuwafikia,” wamesema.


Mwisho, watanzania wote wanaalikwa kuhudhuria siku hiyo, kwani licha ya maadhimisho, Pia, kutakuweo na elimu mbalimbali kama sheria, afya, uchumi n.k. Pia, kutakuwepo na bidhaa mbalimbali kutoka kwa wajane.

0 comments:

HEART OF WORSHIP

HEART OF WORSHIP