25 October 2016

MTAZAMO NA USHAURI WA JOHN PAZIA KWA WAIMBAJI




Anayeonekana kwenye picha hii ni John Pazia, kijana mwenye vipaji vingi, mcha Mungu na mwenye ndoto na maono makubwa

MFAHAMU MTANGAZAJI JOHN PAZIA

John Pazia mwenye makazi yake mkoani Arusha ni mmoja baadhi kati ya watangazaji wenye ushawishi mkubwa Tanzania, na ameinua muziki injili kwa upande wa kaskazini kwa asilimia kubwa na mchango wake umeonekana. Amekuwa sauti ya wengi waliokuwa na kilio cha kuinuka na kutambulika. Ni mtangazaji wa kituo cha radio Radio Habari Maalum kilichopo Jijini Arusha.


MTAZAMO WA JOHN PAZIA KWA MWAKA JANA 2015 NA KINACHOTAKIWA MWAKA HUU
“Mwaka 2015 ulikuwa ni mwaka mzuri ambao ulileta changamoto kwakuwa kuna waimbaji waliofanya kazi nzuri na kuleta changamoto kwa waimbaji wengine, video pia audio na matamasha pia” Alisema John Pazia.
“Pia ulikuwa ni mwaka ambao umewafanya baadhi ya waimbaji wa Injili kujiingiza katika siasa na kuwagawa mashabiki wa muziki wa injili kwa kuingia na kuwaimbia wanasiasa na kuleta gumzo kwa watu na pia gumzo kwa waimbaji wenzao, huenda ikawa walikuwa na malengo yao siwahukumu” na “pia swala la ngazi maana ya makundi ya waimbaji wana mashabiki fulani kama wa Sebene na Hip Hop walikuwa hawachangamani lakini hivi sasa wengi wameanza kuelewa, pia waimbaji wa muziki wa injili wamekuwa karibu wao kwa wao tofauti na kipindi cha nyuma na pia hata kushirikiana katika nyimbo zao.

Pia Wachungaji wameanza kutambua huduma hizi na kukubaliana na kile hususani vijana na kuwaruhusu kumtumikia Mungu katika madhehebu tofauti tofauti na sehemu nyingine nyingi za huduma”. Pia kuna waimbaji waliokurupuka na kufanya kazi mbovu na kutokukubali ushauri, na wengine hawana ushirika mzuri na watangazaji, wengine hutafuta watangazaji wakiwa na shida tu bila hivyo hawana ushirika wa zaidi, wengine hawakubali kuambiwa ukweli wakikosea na hawapendi kuthubutu pia kama kushiriki katika tuzo, pia wengine hawapendi kujitangaza kimitandao, vituo tofauti tofautio vya habari, pia uongozi (management) husema Bwana ataonekana huku wamebweteka, ni jambo la kuthubutu.
Waimbaji wasitoe nyimbo ovyo bila malengo , watazame mbele na pia hii huchangia kutofanya kazi nzuri na zenye viwango, pia video nzuri na zenye viwango.
Pia waimbaji kuwa na ushirika mzuri na makanisa na Baba zao wa kiroho, pia kutodharau waimbaji wadogo ama wenzao lakini ni vyema kuwashauri kwa kutumia njia nzuri ili tuweze kujengana.
Swala muhimu sana ambalo ni vyema watu waelewe si kama wanavyofikiria, uimbaji wa injili ni swala linaloanzia rohoni, na ukitaka wimbo wako usikike  na kuongea na mioyo ya watu na kuponya walioumia, wanaohitaji kutiwa moyo. Usifanye kazi kama kuhudumia watu ila imguse kwanza Mungu na yawe yatokayo kwa Mungu, jenga mahusiano mazuri na Mungu, Mungu hutoa ili awaguse watu wengine kupitia uimbaji.
1.       Ushirika na Mungu, kuomba sana kuliko kuimba sana. Unaweza kutoa nyimbo nyingi lakini zisiguse watu kabisa, kama kiukopi nyimbo za duniani na kuweka maneno ya Mungu kama Mungu haweza kukupa ufunuo.
2.       Waweza kutoa nyimbo nyingi lakini zisiwe na uwepo wa Mungu na Roho Mtakatifu asionekane . Tunza uhusiano na Mungu wako na pia maneno uyazungumzayo kila wakati.

Malengo ya mwaka 2016:
“Malengo ni kuendelea kuusukuma muziki wa Injili na kuwasaidia waimbaji kupitia tasnia yangu, kuwatangazia kazi zao na pia kuwashauri. Haya yote nitayafanya na walio tayari kupokea na kutoa panapostahili, kwakuwa wote tunaujenga mwili wa Kristo. Nitatumia taaluma na kazi yangu kitaifa na kimataifa, nahitaji tu ushirikiano wao” alisema JOHN Pazia.



0 comments:

HEART OF WORSHIP

HEART OF WORSHIP