26 April 2012

UPENDO KILAHIRO APOKELEWA KWA KISHINDO NCHINI CANADA


Mwimbaji nyota wa gospel nchini Tanzania Upendo Kilahiro ameweza kupokelewa vyema nchini Canada huku tamasha lake la kwanza kufanyika jijini Ottawa ndani ya kanisa la Christ Chapel Bible kufanyika kwa mafanikio ikiwa ni pamoja na watu watatu kukabidhi maisha yao kwa Yesu na mwengine akipokea uponyaji.

Tamasha hilo ambalo lengo lake lilikuwa ni kwa ajili ya kukusanya fedha za umaliziaji wa shule ya watoto yatima ya mkoani Morogoro nchini Tanzania iitwayo Dayspring Orphanage boarding school ambayo inafadhiliwa na kanisa hilo,ambapo watu wengi walihudhuria wakiwemo kutoka makanisa ya jirani kama River Jordan Community kwakuwa ni kawaida makanisa jirani kusaidiana na kuwa pamoja kwenye matukio kama hilo,tamasha hilo liliongozwa na viongozi wa kanisa hilo akiwemo Bishop Afolabi,Peter Mwaiteleke huku wageni rasmi walikuwa maafisa ubalozi wa Tanzania nchini humo pamoja na Dada Niku Kyungu Mordi na mumewe ambao hufanya huduma ya kuhubiri huko Maryland Marekani.

                     Bishop Afolabi akimkaribisha Upendo Kilahiro kwa ajili ya kumsifu Mungu.


0 comments:

HEART OF WORSHIP

HEART OF WORSHIP