22 July 2013

UZINDUZI WA KIKUNDI CHA KUSIFU NA KUABUDU KATIKA MKUTANO WA MWINJILISTI BONNKE WAFANYIKA DAR, KARIBU WAIMBAJI 500 WAJISAJILI.

 Zaidi ya waimbaji 500 ktoka kwaya, vikundi na waimbaji binafsi wakiimba kwa pamoja katika uzinduzi wa kuandaa kikundi cha sifa, kitakachotumika kwenye mkutano wa mwinjilisti Bonnke

Mratibu wa mikutano ya Bonnke  barani Afrika, Mwinjilisti Pascal Ado kutoka Togo, akiongea na waimbaji




 Mwalimu John Shabani, akisimamia zoezi hilo

Waimbaji  5000 wanahitajika ili kukamilisha kikundi cha kusifu na kuabudu, kitakachoongoza sifa katika mkutano wa Bonnke, unaotarajiwa kufanyika  kuanzia tarehe 21 mwezi ujao.

Akiongea na mamia ya waimbaji na wanamuziki, mratibu wa mikutano ya Bonnke  barani Afrika, Mwinjilisti Pascal Ado kutoka Togo, amesifia sana uimbaji wa Tanzania na kuwaasa waimbaji kufanya huduma hiyo kwa moyo wote. Amesema mkutano huo utatazamwa  katika nchi mbalimbali duniani, hivyo unadhifu na uchangamfu unahitajika sana. Pamoja na hayo, amependekeza  aina ya nyimbo zinazohitajika na kujiandaa kuwa na sare ya aina ya mavazi ya ki-Afrika


JE WEWE NI MWIMBAJI BINAFSI, KWAYA AU KIKUNDI, UNAKARIBISHWA KUUNGANA NA WAIMBAJI WENGINE KWA AJILI YA KUANDAA TIMU HIYO 

Ni jumamosi hii, pale magomeni mikumi, katika kanisa la T.A.G. Bado tuhitaji waimbaji.

0 comments:

HEART OF WORSHIP

HEART OF WORSHIP