20 March 2012

DON MOEN NA WENZAKE KUPAMBA TAMASHA KUBWA LILILOANDALIWA NA UMOJA WA MAKANISA JIJINI DAR ES SALAAM.



Umoja wa makanisa ya Dar es salaaam ukishirikiana na shirika la kimataifa la LUISPALAU association,liko kwenye mikakati la kufanya tamasha kubwa la injili la upendo maeneo ya Jangwani kuanzia mwezi wa nane hadi mwezi wa 12 mwaka huu, na tamasha hili litafanyika jijini Dar es salaam kama sehemu ya mfululizo wa matamasha ya jinsi hiyo ambayo shirika hilo imekuwa ikiyaendesha katika miji mikuu kadhaa barani Africa.

Kamati ya maandalizi ya tamasha hilo,iliyoundwa na makanisa mbalimbali jijini hapa,tamasha hilo litawaleta nchini wanamichezo mbalimbali wa kimataifa pamoja na waimbaji mashuhuri wa injili,akiwemo Don Moen,Nicole Mullen na wengine wengi,taarifa hiyo imebainisha kuwa wanamichezo wa kimataifa wanaoruka na pikipiki pamoja na baiskeli ya mashirika ya BMX na Fmx nao pia wataalikwa.

Nicole Mullen.
Kwamujibu wa taarifa ya mwenyekiti wa tamasha hilo Askofu Philemon Tibanenason ameongeza kuwa makanisa hayo yamepata fursa ya pekee ya kufanya kazi katika umoja kudhihirisha upendo wa Yesu ubadilishao maisha,tamasha hilo limewahi kufanyika katika miji kama Kigali Rwanda,Bujumbura Burundi,Kampala Uganda na Cairo Misri.

source---gazeti MSEMAKWELI/Gospel kitaa

0 comments:

HEART OF WORSHIP

HEART OF WORSHIP