26 May 2014

DEBORA JOHN HALI YAKE SIO NZURI. SEMA NENO JUU YAKE

Kila unapopiga goti, usisahau kumwambea dada yetu Debora John Said, hali yake bado si swari



Tunahitajika kumuombea ndugu yetu na rafiki yetu Debora John Saidi kwa wakati huu mgumu anaopitia. Hiki ni kipindi kigumu sana kwake kwania anateseka sana na maumivu makali. Mwimbaji huyo wa Injili na mama Mchungaji John Saidi, ambaye hali yake inaelezwa kwamba si nzuri na sasa yuko chumba cha upasuaji hospitali ya Mwananyamala kuondolewa uvimbe mkubwa tumboni ambao umesababisha asumbuliwe na maumivu makali yanayosababisha atokwe na machozi mara kwa mara.

Wito wetu kwa watumishi wa Mungu, tamka neon moja mbele za Mungu kwa ajili ya uponyaji wake; pia panga kumjulia hali.

0 comments:

HEART OF WORSHIP

HEART OF WORSHIP