2 June 2014

UMUHIMU WA KUJIUNGA NA CHAMA CHA MUZIKI WA INJILI TANZANIA



Mkutano wa waimbaji,wanamuziki na wadu wa muziki wa Injili uliofanyika mwaka juzi katika hoteli ya wanyama iliyopo Sinza, Dar. Kongamano hilo lilikua lilifadhiliwa na mfuko wa jamii NSSF





 Ziara ya uongozi wa chama cha muziki wa Injili na wadau wengine, kuwatembelea watoto yatima huko mkuranga


 Uongozi wa chama cha muziki wa Injili walipomtembelea mzee Makasy

                                         Ziara ya kuhamasisha chama mikoani

Uongozi wa chama cha muziki wa injili wakimpongeza Bw. Msama

Mmoja wa wanachama, Bw. Magida Timotheo akiwa ameshikilia katiba ya chama



Moja ya sababu za msingi kutuweka pamoja waimbaji na wanamuziki wa injili, ili tuwe na sauti moja katika kutetea na kusimamia haki za waimbaji/wanamuziki na kila anayehusika na muziki wa injili nchini na pia ni agizo la serikali kwamba, waliona kwa sababu muziki wa injili unauzwa dukani kama miziki mingine kwa hiyo kitu chochote kikishauzwa dukani lazima kiwe na sheria zake na kikishakuwa na sheria zake lazima kiwe na haki na wale wanaofanya zile kazi wawezekujua faida zake na wawezekufaidika na zile kazi zao
Pia ni kwamba baada ya kuona sanaa ya muziki inakua kwa kasi hivyo ikaonekana kuna umuhimu wa kuwepo na shirikisho la muziki Tanzania kama vile ilivyo shirikisho la mpira (TFF). Hivyo basi shirikisho hilo lianundwa na vyama vilivyosajiliwa. Najua vipo vikundi vingi vinavyounda umoja wa waimbaji kutoka makundi ya aina fulani ya muziki, lakini ukweli ni kwamba, vyama vya muziki vinavyotambuliwa na serikali ni vile vilivyosajiliwa kihalali na kupewa kibali kupitia Basata (Baraza la sanaa la taifa), na moja kati ya vyama vyenye kibali cha serikali ni chama cha muziki wa Injili Tanzania (CHAMUITA) chenye usajili: BST 4598  .  Najua waimbaji wa injili nchini wakiwemo wanamuziki, maproducer na wapenzi wa nyimbo za injili wanaweza kuwa na maswali mengi kuhusu chama hiki, pia kuwepo na hali ya kusitasita kujiunga, lakini huko tunakoelekea kuna watu watajua umuhimu wa kujiunga na chama. Si vibaya kuhoji, lakini ipo katiba inayotambulika na serikali, hivyo basi ni wajibu wa kila mwanachama hai kuwa na nakala ya katiba hiyo.
Ni wito wangu kwa kila mtu anayehusika na muziki wa injili Tanzania, uwe mwimbaji, mwanamuziki, mwinjilisti, mchungaji, producer, Mc na mpenzi wa muziki wa injili, kujiunga na chama na kuwa na kitambulisho chake halali kama mwanachama wa muziki wa injili Tanzania. Lakini pia ikumbukwe jambo peekee alilolisema yesu muda mfupi kabla hajapaa mbinguni, aliagiza upendo. Hivyo sioni sababu ya waimbaji kutokuwa wamoja, kutokupendanda, kuweka matabaka, kutokubebana na kuinuana. Ebu tuamke, tusiishie kuandaa matamasha ya kujipatia pesa, lakini tusimame katika agizo kuu la kuwaleta watu kwa Yesu. Tunaweza kabisa kuandaa mikutano mikubwa ya injili na makongamano, tunaweza kabisa kutenga muda wa kufunga na kuomba pamoja; na huu ndio wakati, tusisubiri kusikia tu habari mbaya za mpendwa mwezetu na kuzishabikia, tumeagizwa upendao!
Chama cha Muziki wa Injili kilianzishwa mwaka 2011,Uongozi wa chama cha Muziki wa Injili Tanzania, Mwenyekiti ni Addo November, katibu anayekaimu ni John Shabani,katibu mwenezi ni Stella Joel,Mwekahazina ni Upendo Kilahilo.. Idadi ya wanachama waliojiunga kwa Dar es Salaam wanakaribia kuwa elfu nane, Morogoro na Pwani ni mia tatu na Arusha na Kilamanjaro viongozi ndo wanahamasisha wanachama kujiunga ...Tuna kanda kama nne ambazo zinaviongozi kanda ya kaskazini inayojumuisha Tanga,Kilimanjaro,Arusha na Manyara mwkt ni Samweli Nungwana katibu ni Anne Annie,Morogoro na Pwani kiongozi ni Ester mwamboma na wengine,Kanda ya ziwa kiongozi ni Jacob Mutashi na Kanda kusini pia wapo viongozi wao. Jinsi ya kujiunga kwenye chama cha muziki wa injili kuna Ada ya uanachama utajiandikisha kwa Tsh 20000/= na utatengeneza kitambulisho kizuri kwa Tsh 10000/= kwa hiyo ni muhimu sana waimbaji na wanamuziki wa injili Tanzania wakajiunga kama unavyojua mwanachama hai ni yule anaelipa Ada ya kila mwaka, ukishalipa ada unakuwa na sauti ndani ya chama unakuchagua au kuchaguliwa na unaweza kufaidika na faida zote zinazotokana na Chama cha Muziki Wa Injili Tanzania.

0 comments:

HEART OF WORSHIP

HEART OF WORSHIP